أول 200 سطر.
Ninajua kila kitu.
Ninajua kila kitu sasa.
Rain...
Sielewi. Unajua nini?
Ninajua nimekosa. Lakini sielewi. Unasema nini?
Raina, niambie.
Najua si kumhusu Mitha tu. Lazima kuna jambo lingine.
Najua kila kitu.
Najua mbona umebadilika.
Najua mbona hukunikubali kwanzia mwanzo,
na mbona uliamua kusaliti ahadi uliyompa Dimas.
Si kwa sababu hunipendi.
Unajua nini?
Nashukuru kuwa mamako aliniambia nije huku.
Rain, kusema ukweli sielewi unachosema.
Lakini hangekutuma huku.
Nilimpigia simu kila siku kumwambia kuwa nilitaka tutengane.
Ndiyo maana nimesikitikia sababu iliyomfanya akakumuma huku bado.
Mamako anajua?
-Kujua nini? -Nijibu Rangga.
Unamaanisha nini kuwa umebadili uamuzi wako
na unataka kutengana na Raina?
Mama.
Nimefanya kile ambacho Dimas aliniambia nifanye, kumchunga Raina.
Sasa tunaishi maisha yetu binafsi.
Nimefanya kosa lipi?
Rangga, huwezi kufanya hivyo. Huwezi kufanya unachotaka tu.
Rangga.
Nakujua.
Hii si tabia yako ya kawaida. Niambie.
Tatizo lako ni lipi?
Mpendwa, ni nani?
-Rangga, huyo ni nani? -Hakuna.
Kwa hivyo hilo ndilo tatizo? Umepata msichana mwingine huko?
Usimdanganye mamako.
Mama, sivyo.
Ukweli ni kuwa,
huwezi kutengana na Raina.
Ni lazima mwendelee.
Siyo kuhusu kile ambacho Dimas anataka tu.
Lakini ni kuhusu wewe na Raina.
Sitakuruhusu utengane na Raina kwa urahisi.
Hilo linamaanisha kuwa shangazi Cindy hajui?
Ndiyo maana aliniambia nije huku.
Najua kila kitu. Najua kila kitu.
Hujambo? Naweza kukusaidia?
Hawa ni mabinti wako?
-Ni warembo. -Ndiyo.
Ni mabinti wangu.
Asante.
Nina hakika kuwa...
...unanijua.
Mimi ni Dahlia.
Ninafikiri,
hakuna mtu yeyote anayeweza kusahau
chanzo cha uchungu katika maisha yake ya awali.
Sivyo?
Imekuwa miaka 19.
Umekuwa ukiangamiza maisha yangu.
Kunidhuru hapa na pale.
Bado inaniuma.
Unataka nini?
Hujakuja kununua haya maua maridadi kutoka kwa Flora.
Nitasema hivi.
Nimekuja kukutafuta.
Kwa sababu nataka kumuona binti yangu Kinara.
Kinara? Binti yako?
Ndiyo.
Sijamwona binti yangu kwa muda wa miaka 19.
Mbona unaniuliza kuhusu binti yako?
Unadhani ulimpeana mwanao lini?
Nilimwacha Kinara na babake,
nilipoamua kutengana na Surya.
Nina uhakika kuwa,
kabla Surya afe,
ni lazima alimkabidhi Kinara kwako.
Yaani unamchukulia mtoto kama kitu, sivyo?
Ulininyang'anya mume. Ukamzalia binti.
Na sasa umekuja hapa ghafla,
kuniuliza kuhusu binti yako.
Itakuwa vyema uende kwa daktari wa magonjwa ya akili.
Nakutakia afueni ya haraka.
Nimegundua kuwa,
si muhimu kupiga magoti na kukuomba msamaha sasa hivi.
Surya ameaga.
Nakusihi.
Kwa vyovyote vile, mimi ni mama mzazi wa Kinara.
Nina haki ya kujua aliko.
Nina hakika amekuwa akiishi na wewe.
Unajua maana ya kuwa mama?
Mama huugua, mtoto wake anapougua.
Huwa anauliza mtoto wake kama ameshiba, kama anataka chakula zaidi.
Huwa anampatia mtoto wake kila kitu.
Si kumtelekeza.
Mwanamke kama wewe hawezi kujiita mama,
wala kuzungumza kuhusu kuwa mama.
Mimi si mwanamke mzuri.
Mimi si mama mzuri. Siwezi kuitwa mama.
Lakini Kinara ni mtoto wangu.
Ulimbeba tumboni na ukamzaa.
Ndiyo, yeye ni mtoto wako, lakini ulimtelekeza.
Tafadhali nakusihi.
Niruhusu nirekebishe makosa yangu ya awali.
Surya alisema ukweli.
Wewe ni mwanamke anayeheshimika sana.
Na una moyo safi.
Usimhusishe mume wangu.
Mungu amemlaza mahali pema peponi.
Ninajua.
Kwa sababu ya ukarimu wako,
umekuwa tayari kumchunga Kinara.
Kwa hivyo nina uhakika,
utampa Kinara fursa ya kuonana nami.
Awe anataka kunichukia,
kunilaani au kulipiza kisasi, mruhusu.
Kwa sababu ana haki ya kunitendea hivyo.
Nijibu tafadhali.
Kati ya hawa wasichana wawili, Kinara ni nani?
Wote wawili ni mabinti zangu.
MAGIC HOUR THE SERIES
Tukio la 6: Kumpenda mtu au kupendwa
Nimegundua kuwa
maisha ni hiari.
Na tuna hiari mbili.
Kupenda
au kupendwa.
Kama ninaweza kuchagua,
sitalichukulia kama chaguo.
Kwa sababu nataka kupenda na kupendwa. Nataka yote.
Ninapoyataka yote mawili, nagundua kuwa si hiari tena.
Bali ni baraka.
Rangga, ndiyo maana ninavumilia.
Na...
Na leo
hatimaye nimepata jibu.
Jibu ambalo limekuwa likinisumbua
tangu siku yangu ya kwanza kuingia New York.
Jibu ambalo sitapata kutoka kwako.
Sehemu za fumbo ambalo linanifanya niendelee kuwa nawe.
Lakini nimepata utulivu,
hujabadilika kwa sababu hunipendi tena,
au kwa sababu ulimtia Mitha mimba.
Lakini kwa upande mwingine ninajiuliza.
Ingekuwa vyema kama sababu ingekuwa hunipendi tena?
Rain, unajua nini kunihusu?
Unamaanisha jibu lipi?
Nitarudi nyumbani nilivyokuahidi.
Lakini hiyo ndiyo sababu ningali niko hapa.
Sijali. Niko tayari kuhisi uchungu huo tena.
Ilimradi niko nawe
na uko nami daima.
Hadi pale kutakuwa na uamuzi mwingine wakati unavyosonga.
Mbona umekuja tena?
Nilidhani hukutaka kuniona tena.
Baada ya kutengana,
haimaanishi kuwa hatuwezi kuwa marafiki, sivyo?
Pia haimaanishi kuwa,
nimeacha kukujali.
Mbona?
Nilikukosea sana.
Nilizini. Nilikuvunja moyo.
Mbona unanijali?
Inawezekana kuwa,
ungali unanipenda?
Kukupenda?
Mitha.
Katika maisha haya,
hatuwezi kupima kinachofanyika katika hali ya mapenzi,
chuki, kupenda au kutopenda.
Katika hali hii,
mimi ndiye nilikuwa na uhusiano na wewe.
Na nilijiahidi kuwa nitakuchunga daima.
Lakini mimi ni mjamzito.
Na si ujauzito wako.
Na sasa unazungumzia kuwajibika. Mimi...
Mitha, hebu jiulize.
Ulifanya hivi kwa sababu hunipendi?
Kwa sababu unanichukia?
Kama ni kweli kuwa hujawahi kunipenda,
mbona hukutengana nami,
kabla uwe na uhusiano na Rangga?
Sababu yako ni ipi?
Mitha,
siwezi kubadili kilichofanyika na
hilo silo ninalotaka. Lakini uamuzi ni wako.
Na mimi nina haki ya kuchagua.
Angalau,
hadi wakati ule ambapo baba ya mtoto aliye tumboni mwako,
atawajibika.
Hujui, sivyo?
Mtazamo wako unanifanya nihisi kuwa na hatia hata zaidi.
Nahisi kuwa nilikufanyia jambo baya zaidi.
Wewe ni mwathiriwa
wa mwanamume mbaya.
Kwa hivyo,
niache niwe nilivyo.
Iwapo hutaki nikufanyie haya,
nitamfanyia mwanao.
Rangga atakapowajibika,
nitatoka maishani mwako.
No comments yet. Be the first to leave one.