أول 200 سطر.
Baba tafadhali usikasirike.
Nitakueleza suala lote.
Jana kaka Nasir alikuja.
Bila ya kukutana nami, bila idhini yangu, akaondoka hapa?
Nilichukulie kama kunikosea heshima, kutotii au uasi?
Hapana baba.
Hasira yako inaeleweka, Sultani.
Lakini tafadhali fanya uamuzi wako baada ya kufikiria.
Hakuna cha kufikiri au kuelewa.
Mimi, Sultan-E-Hind, Iltumish, ninakabidhi cheo cha Subhedar wa Delhi
kwa mwanangu, Mwana Mfalme Ruknuddin.
Asifiwe Mwana Mfalme Ruknuddin.
Asifiwe Mwana Mfalme Ruknuddin.
Asifiwe Mwana Mfalme Ruknuddin.
Asifiwe Mwana Mfalme Ruknuddin.
Asifiwe Mwana Mfalme Ruknuddin.
Asifiwe Mwana Mfalme Ruknuddin.
Asifiwe Mwana Mfalme Ruknuddin.
Asifiwe Mwana Mfalme Ruknuddin.
Asifiwe Mwana Mfalme Ruknuddin.
Uamuzi mmoja mbaya tu, na kila kitu kiliharibiwa.
Ufalme wa Delhi ambao ulikuwa haki
ya warithi wa mume wangu Qutubuddin....
...Sultani Iltumish ametoa haki hiyo
kwa mwana wa kahaba,
na kuangamiza ukoo wa ufalme.
Kuna nini cha ajabu hapo, mama?
Hii si mara ya kwanza kwa Sultani Iltumish kufanya kitu kama hiki.
Alimnyang'anya kaka yetu Alam Shah haki yake hivi.
Kimya, Uzma.
Huu sio muda wa kutonesha vidonda vya zamani.
Mambo yaliyosahaulika, yaache hivyo.
Kwa nini nikae kimya?
Vidonda vitatoneshwa.
Hata kila mtu akijaribu kulizuia.
Sote tunajua kuwa mrithi halisi wa ufalme wa Delhi alikuwa kaka yetu,
Alam Shah.
Nitawezaje kusahau?
Nitawezaje kusahau kwamba kiti cha enzi kinachokaliwa na Sultani Iltumish...
kiti hicho cha enzi kina alama za damu ya kakangu.
Kila mmoja pia anajua ukweli, Uzma...
hali ambayo ndugu yetu alifariki.
Licha ya ukweli kwamba alikuwa ndugu yetu,
pia ni ukweli kwamba hakuwa mtu mzuri.
Alikuwa mlevi sugu na mtu mharibifu.
Na chaguo la kwanza la baba yetu lilikuwa Sultani Iltumish pekee.
Sasa haya yametosha.
Mwanangu aliuawa nikabaki mama mwenye huzuni.
Lakini tutapata faida gani kwa kujadili suala hili sasa?
Nashangaa, mama mkwe mpendwa.
Ninashangazwa na namna unavyoweza kumstahimili Sultani Iltumish
ambaye alikuwa muuaji wa mwanao.
Historia inajirudia.
Sultani Iltumish ananyakua haki ya mjukuu wako mpendwa tena
na kumpa huyo Ruknuddin.
Na wewe bado unamtetea?
Hakuna haja ya kuongea kuhusu masuala ya kale, mjomba.
Licha ya hali iliyopo,
siko tayari kusikiliza hata neno moja dhidi ya baba.
Tulikubaliana kwamba kilichotokea kilikuwa kosa.
Lakini namjua baba yangu.
Lazima kuwe na sababu ya jambo hilo.
Na hiyo sababu itajitokeza wakati mwafaka utakapofika.
Na kuhusu kutosikizana kati yangu na baba,
baba na mwanawe wanaweza kuelewana na kupungiza kutosikizana huko.
Njoo, mpendwa wangu. Njoo unikumbatie.
Koma, Nasir.
Ni vizuri kwamba umewasili sasa, baba.
Alinishinda kwa njia haramu katika mashindano hayo
Kwa kuharibu ukanda wa Rustom.
Mchezo wako sasa umeisha, Nasirmiya.
Ninamshukuru Mungu kwamba nilijua kuhusu njama mliyokuwa mnapanga
na nilimwambia Sultani kabla ya haya yote.
Uchungu si kuhusu jinsi Nasir alikuacha kwa hasira..
lakini jambo moja linalonipa wasiwasi
ni kuwa hii inaweza kuwa hatua yake ya kwanza katika uasi?
Umeshindwa katika shindano hilo.
Sasa unataka kupoteza upendo wa babako pia
kwa sababu ya uongo?
Baba.
Ukikasirika hivi, basi tutafanya nini?
Angalau sikiliza nitakayosema.
Kaka Nasir hakutaka kwenda.
Kwa nini kakangu tu? Bibi, mama... hakuna aliyetaka kuondoka kwa njia hii.
Lakini hali ilikuwa ilikuwa hivyo.
Usiwatolee kisingizio kwa kuchukulia ufidhuli wao kama udhaifu, Razia.
Baba, sitoi kisingizio kwa mtu yeyote.
Ninasema ukweli tu.
Nina ombi moja tu kwako, baba.
Kama hili ni kosa lao, basi tafadhali wasamehe.
Tafadhali nipe ruhusa ya kuwarejesha.
Kama wakati wa kuondoka hawakuomba ruhusa
basi kwa utake warudi?
Baba, kwa sababu kila mtu anakupenda sana.
Ukiwarejesha, basi upendo wako kwao wataushuhudia.
Wana haki hiyo, sivyo?
Na kama wangeichukua kama haki yao,
basi wangefikiria kabla ya kuondoka.
Kwa nini unataka niwarejeshe?
Waliondoka kwa hiari yao kwa hivyo acha warudi kwa hiari yao.
Baba.
Mikono inayotumiwa kunoa almasi na kuifanya ing'ae
ndiyo hiyo hiyo inayoshindwa kuiboresha.
Mgogoro unaoendelea ndani ya moyo wako
unaonyeshwa na mikono yako, baba.
Baba, tafadhali okoa familia yetu isisambaratike.
Tafadhali waite wote nyumbani.
Unaweza kunoa almasi hii na kuifanya ing'ae zaidi.
Yale Mwana Mfalme Nasir amefanya hayastahili kusamehewa.
Lakini kwa sababu ni ombi lako, basi nitampa fursa moja ya mwisho.
Asante sana, baba.
Lakini kumbuka kwamba hii ni fursa ya mwisho.
Martand.
Mfalme mkuu.
Enda Multan mara moja
na umshukuru Sultani Khawaja kwa niaba yangu kwa kukaribisha familia yangu kwake.
Pia wasilisha amri zangu kwa Mwana Mfalme Nasir na mamake...
kwamba wanaweza kurudi Delhi wakitaka.
Hakuna haja ya kuwaomba.
Tafadhali wasilisha ombi mara moja tu.
Aidha, baba, unajua kwa nini nilibaki hapa?
Kwa sababu sikutaka kwenda kukuacha peke yako hapa.
Lakini angalia, kama ningeenda Multan pia,
ningekutana na shangazi Uzma na kila mtu huko.
Ingefurahisha sana.
Tafadhali sema wazi kile unachotaka kusema.
Baba, kama bwana Rana ataenda Multan, ataenda kwa misafara, au siyo?
Machela tupu zitaenda, misafara tupu itaenda.
Kwa hivyo nilikuwa nafikiri kwenda kwa misafara hiyo mwenyewe.
Kwa njia hii nitakutana na kila mtu na itakuwa safari nzuri kwangu.
Basi unaniomba ruhusa ya kwenda Multan?
Hiyo pia peke yako?
Wapi peke yangu, baba?
Bwana Rana atakuwa na mimi na ninajua
unamwamini kabisa kuhusu usalama wangu.
Sasa ikiwa si kama baba, unaweza
kutimiza matakwa yangu kama Mfalme Mkuu, sio?
Sawa. Unaweza kwenda.
-Rana Martand. -Ndio Mfalme Mkuu.
Tafadhali mchunge vizuri Binti Malkia Razia.
Ndiyo, Mfalme Mkuu.
Baba, wewe ni mzuri sana.
Hakuna baba mwingine mzuri kama wewe katika ulimwengu wote huu.
Sasa nitachukua idhini yako, baba.
Lazima nifanye mipango nyingi kwa ajili ya safari.
Mungu akubariki.
Wewe kweli huna subira, mpendwa.
Hujui kwamba baada ya pombe kukunyiwa,
inaacha alama.
Matokeo hayo yanaanza kuongezeka, mama.
Kuna shangwe kila mahali, shangwe kila mahali.
Basi mtu yeote atajuaje kuihusu, kuuliza nani amekunywa?
Mwanangu, kila mtu hunywa kwa midomo yao,
lakini ni mimi ninayelewesha kila mtu kwa macho yagu.
Kwa hivyo tosti huu unapendekezwa kwa jina lako, mama.
Kwa nini kwa jina langu?
Pendekeza kwa majina ya wale wanaoenda Multan.
Unamaanisha nini?
Sultani amewatuma Razia na Martand hadi Multan.
Ili kuleta Nasir hapa.
Vizuri, vizuri.
Habari gani umenipea, mama.
Habari gani umenipea.
Acha huyo Nasir arudi.
Ana madharau mengi, sivyo?
Mimi ni Subhedar wa ufalme huu, mama.
Kama sitamfanya abebe viatu vyangu, unaweza kubadilisha jina langu, mama.
Hicho ndicho hasa unakosa, mwana.
Hapa ninaota ya kukufanya uwe Sultani.
Na wewe unapiga tarumbeta kuhusu kuwa Subhedar?
Unajua hata viatu vinaweza kuwa taji kichwani siku moja.
Sikuelewa ulichomaanisha, mama.
Tafadhali kumbuka mwana kwamba ulishinda mashindano haya kwa uongo
na si kwa ujasiri.
Nasir ni mwanajeshi aliye na kipaji sana.
Hakuna anayetilia shaka uwezo wake.
Wakati wowote, anaweza kuwa mwasi.
Lazima tumwangamize kabisa.
Lakini mama, tutawezaje?
Kaa macho tu.
Hatua ya mwisho ya mchezo bado haijachezwa.
Lakini kabla ya Binti Malkia Razia aende Multan,
niruhusu kutimiza majukumu yanayohusika na mahusiano.
Na unafahamu vizuri kuwa ninaweza kudumisha mahusiano.
Kama ni ya urafiki au uadui.
Ni hayo tu.
Kuna nini, kaka Zaroon?
Ni hofu gani imekufanya ugeuka kuwa manjano kama pea?
Kula hii na rangi ya uso wako itarejea.
Miya, maisha yetu yako hatarini hapa,
na unachofanya ni kula peremende tu?
Ziangalie tu, kaka.
Jinsi zinakutazama kwa macho ya shira.
Angalia jinsi inavyovutia.
Hiki kiuno, huu mwili wenye harufu nzuri.
Chukua, ule.
Nakuahidi utashangaa sana.
Miya, jeshi lote la mkuu linatutafuta
na huna wasiwasi wowote usoni mwako?
Zaroonmiya, ni wewe unayefikiria kila mara kuhusu zamani na siku za usoni.
No comments yet. Be the first to leave one.