أول 187 سطر.
Kila wakati unadhihirisha huu ukweli, Sultani.
Kuwa niliazimia kuwa mkeo usiku na mchana.
Lakini kudra pia hucheza michezo kama hiyo.
Sikujua kuwa kwa kifo cha mwanangu
ambaye hakuwa amezaliwa,
ningevishwa kama bibi harusi.
Anaweza kuwa wapi mama aliye na bahati mbaya kama mimi?
Yule ambaye machela ya harusi yake inabebwa na mwili wa marehemu mwanawe.
Usihuzunike sana, Turkan.
Sielewi maumivu yako.
Inaniuma sana kuwa haya maumivu yameletwa kwako na jamaa wangu.
Nilikuwa nikifikiria kuwa mimi ndiye mtu wa ajabu pekee humu duniani,
lakini wewe ni zaidi ukilinganishwa na mimi.
Bibiye, sasa usiponiambia tatizo, nitakusaidia vipi?
Hakuna yeyote kando na Sultani Aldos wa Ghazni
anaweza kunisaidia.
Nini? Sultani Aldos?
Unasema nini?
Mbona huyo Sultani maarufu Aldos atake kukusaidia?
Sahau kuhusu kusaidiwa. Haiwezekani kukutana naye
kwa watu wa kawaida kama sisi.
Nieleze au niseme nini,
ilihali hajui chochote kunihusu?
Itabidi niende sasa.
Kwaheri.
Kuwa mwangalifu.
Sultani Iltumish, ndoa yako na shah Turkan iko karibu kufungwa.
Je, unakubali hii ndoa?
Nyamaza, wewe mwanamke msherati.
Lo! Sultani! Mwanangu!
Yeye sio mumeo wala babangu.
Yeye ni mpenzi wa huyu kahaba tu.
Nakubali.
-Unakubali? -Ndiyo.
-Unakubali? -Ndiyo.
Shah Turkan, uko karibu kufunga ndoa na Sultani Iltumish.
Je, unakubali hii ndoa?
Nakubali.
Nakubali.
Hongera, hongera!
Pongezi kwenu!
Ni kama nimepotea njia.
Nimeshindwa kuelewa ni njia gani itaelekea Ghazni.
Ramani.
Niliweka wapi ile ramani?
Hiyo ramani, nadhani niliiacha kijijini.
Mungu, ewe mungu, hali hii ni mbaya sana.
Nisipopata hiyo ramani, nitafikaje Ghazni?
Na nisipofika Ghazni, ni vipi nitasitisha vita?
Ewe mwenyezi Mungu, nisaidie tafadhali.
Nisaidie, la sivyo kila kitu kitaharibika.
Nitajuaje njia inayoenda Ghazni?
Msafiri asipojua njia inayoenda anakoenda bibiye,
anawezaje kufika anakoenda?
Hii ni sauti ya Mirza.
Lakini Mirza anawezaje kuwa hapa?
Unadhani wewe ni mwerevu sana, sivyo?
Unaweza kuona ninavyosumbuka.
Na wewe umeketi hapa tu kunipa ushauri?
Kama kumwonyesha msafiri aliyepotea njia ni ushauri,
basi unaweza kuchukulia kama ushauri bibiye.
Sasa badala ya kunishukuru, unanikasirikia?
Mtu huonyesha hasira kwa watu anaochukulia kuwa karibu naye.
Kweli?
Lakini mimi nina uhusiano gani nawe?
Naweza kukuua wewe pia.
Upendo ulioje!
Hata kama wewe sio mwenyeji,
bado unaweza kutekeleza majukumu yako kama mwanaume mwenye adabu.
Nataka kufika Ghazni haraka iwezekanavyo.
Je, utanionyesha njia?
Nifanyie huo msaada mdogo tu.
Nafurahia hasira yako zaidi ya ombi lako bibiye.
Lakini nitakupa ushauri mmoja zaidi.
Habari ikibadilika, acha ibadilike lakini utendaji usibadilike.
Usiombe tafadhali.
Unavutia ukiwa mjeuri.
Sikiliza, acha kupayuka na uende nami,
la sivyo, nitakuning'iniza kwenye huu mti ukiwa umeangalia chini.
Haswa.
Sasa kiburi kimemzidi mwanakondoo.
Ulimuita nani mwanakondoo?
Bibiye, hiyo ilikuwa njia ya kusema tu.
Vinginevyo, ningewezaje kukwambia jambo?
Sitaki kukatwa kichwa, sivyo?
Kuja tafadhali.
Niseme jambo moja?
Unaweza kusema mambo mawili.
Hakuna mpaka kwa mazungumzo, sivyo?
Usiniite binti mfalme tafadhali.
Sipendi kabisa.
Kweli?
Niambie ukweli.
Hupendi au una wivu?
Ili ufurahi, unaweza kuamini unavyotaka.
Unavyoamuru, binti mfalme. Sitakuita hivyo tena,
binti mfalme.
Mtu anapata lulu bila kuomba.
Wakati mwingine hupati hata ukiomba.
Mungu amenijaza furaha nyingi sana,
ambayo sikuwa nimewahi kufikiria.
Nimegeuka kuwa malkia kutoka kwa kuwa kahaba.
Mwanangu Ruknuddin amekuwa kiongozi wa jeshi.
Na Sultani Iltumish anataka kumwaga damu ya mwanawe mwenyewe.
Na jambo bora zaidi, ni kuwa binti mfalme Razia amekufa sasa.
Mungu wangu! Siwezi kustahimili hii furaha yote.
Mama, mama.
Nataka kuongea nawe kuhusu jambo muhimu sana.
Kuna habari mbaya.
Una tabia mbaya.
Siku zote huwa unaleta habari mbaya kwa hafla yenye furaha.
Simamisha machela.
Mama, ni mbaya sana.
Nimebaini kutoka kwa wapelelezi wetu kuwa Jangura ameuawa.
Hilo linawezekana vipi?
Jangura anawezaje kufa?
Hata mimi sikuamini mwanzoni,
lakini habari imethibitishwa.
Maiti imepatikana mbugani.
Hili linamaanisha kuwa Razia angali hai.
Na hakuna wa kumkomesha kwenda kukutana na Sultani Aldos jijini Ghazni.
Hilo ni dhahiri, mama.
Huu ndio mpaka wa Ghazni? Bado siwezi kuamini macho yangu.
Bibiye, unaweza kuona huo mlango?
Ili kuingia kwenye huo mlango, itabidi tuwahadae wale walinzi.
Na unafahamu vizuri jinsi ambavyo huwa nahadaa watu.
Nisubiri hapa.
Nitaenda hivi na kurudi vile.
Wewe, nisikilize.
Hawatakuruhusu kuingia kwa njia yoyote ile.
Kipenzi, mimi ni mtu anayeweza kupita kwa mtu mwingine,
bila yeye kujua.
Huo ni mlango tu.
Tazama muujiza wangu.
Huyu mwanaume, ni Mungu anajua anavyofikiria kujihusu.
Hata hivyo, hata awe nani, acha tuone.
Lakini huyu mwanaume ni mwerevu sana.
Ajuaye ni nani? Huenda naye akafanikiwa.
Tutakuzika ardhini, ukijaribu kuingia kasrini bila idhini.
Sitafanya hivyo, sitafanya hivyo.
Hapana, mimi ni mtu anayeweza kupita kwa mtu mwingine
bila yeye kujua.
Na huo ni mlango tu hata hivyo.
Au sivyo?
Angalia muujiza wako sasa.
Jamani, hao wawili walielewa vibaya.
Sababu ni kwamba kuna tofauti kwa lugha zetu.
Kusema ukweli wangekuwa wamenibeba kwa mabega yao kwa heshima,
na kunipeleka nkwenye kasri.
Lakini sijui mbona waliniweka hapa.
Sasa usijigambe sana Mirza. Umetambulika.
Jamani, kipenzi!
Mgongo wangu umeteguka.
Bibiye, kusema ukweli, sikufanya chochote kwa sababu yako tu.
La sivyo, ningekabiliana vilivyo na hao wapiganaji.
Shika, nipe mkono wako.
Huwa husikilizi, Mirza.
Nilikuwa nimekuomba uniruhusu niende huko.
Bibiye, nisikilize.
Wewe pia usiende huko, la sivyo, utakuwa matatani hivi.
Nilimaanisha kuwa urudi na mimi.
Sijakuja umbali huu ili kurudi, Mirza.
Naenda ndani.
Utanisubiri hapa?
Mungu wangu, Mungu wangu, Mungu wangu.
Sikiliza bibiye.
Wewe ndiye kiu yangu na wewe ndiye ziwa langu,
wewe ndio njia yangu ya kupata amani.
Kivuli chako kinafaa kuwa kwa nafsi yangu,
hatima yako inafaa kutokana nami.
Kivuli chako kinafaa kuwa kwa nafsi yangu,
hatima yako inafaa kutokana nami.
Utaingia ndani tu, ukiacha mkono wangu, sivyo?
Baraka zako kwetu ni maarufu sana.
Nafsi yangu inazitegemea.
Wewe ndiye ombi, wewe ndiye Mungu, wewe ndiye kosa, wewe ndiye adhabu.
Popote pale macho yangu yanapoangalia, huwa unakuwepo siku zote.
Mungu wangu, Mungu wangu, Mungu wangu.
Mungu wangu, Mungu wangu, Mungu wangu.
Asante kwa kila kitu, Mirza.
Fungueni mlango mniruhusu niingie.
Nataka kukutana na Sultani Aldos.
Tazama huyu.
Tumemfukuza mjinga yule na sasa huyu msichana mwendawazimu amekuja,
kukutana na Sultani Aldos.
Lazima huyu msichana mwendawazimu naye yuko tayari kutoa maisha yake mhanga.
Mimi ni wako, kipenzi. Kwa hivyo, Mirza naye atakufwata.
No comments yet. Be the first to leave one.