أول 200 سطر.
Delhi. Moyo wa India, Delhi.
Na kuna pigo la moyo huu, Qutub Minar.
Mtu ambaye ameona falme nyingi zikifaulu na nyingi zikianguka.
Hadithi hii ni ya wakati warithi wa Ghulam walikuwa wakitawala nchi hiyo.
Kabla ya kuwasili kwa Wamughal miaka mingi iliyopita,
asili ya hawa watu ilikuwa katika karne ya 12
ya Sultani Qutubuddin Aimatullah.
Wakati kulikuwa na jeraha na alama za mateso kwa miili ya watumwa.
Na ilikuwa kawaida kwao kuuzwa na kununuliwa kwa soko wazi.
Wakati kama huo, mtu atasema nini kuhusu utambulisho wa wanawake?
Na kwa mwanamke kuwa Sultani lilikuwa jambo lisiloweza kuwazwa.
Lakini nyakati zilikuwa zinabadilika muda ulivyosonga.
Na mwanzoni ilikuwa inafanywa na Sultani kama huyo
ambaye baadaye aliwapuuza wanawe wa kiume
na akapendelea kuucha ufalme mikononi mwa binti yake.
Kwa historia huyu Sultani mkarimu alijulikana kama Iltumish.
Aishi maisha marefu Sultani.
-Bismillah Rehmat Rahim. -Asifiwe Sultan.
Kwa uwezo wake ufalme wetu umelindwa.
Na nguvu za ufalme huu uko kwa upendo mkuu wa watu wake.
Hivyo mimi ndiye Sultani wa nyinyi watu.
Lakini niaminini kuwa mimi ndiye mtumishi wenu mkarimu.
Fanaka yenu ni wajibu wangu.
Na usalama wenu ni lengo langu.
Leo mwezi utaonekana.
Na ninatamani pia kuuona mwezi katika siku ya Eid.
Kwa hivyo nimeamua kuwapa watu wa ufalme wangu zawadi siku hii maalum.
Kweli vyema.
Kwa kusimamisha ushuru wa sarafu ghali za dhahabu za zamani
na nimeamua kuzibadilisha na sarafu za fedha bei ra zahisi.
Badala ya sarafu moja ya dhahabu,
unaweza kupeleka sarafu 10 za fedha kwa Hazina ya Kifalme.
Aishi maisha marefu Sultani.
Aishi maisha marefu Sultani.
Aishi maisha marefu Sultani.
Nitatangaza kwa umma kwa kushuhudia mwezi wa Eid
kila mtu atachukua jukumu la kusoma aya kadhaa,
watatuzwa kwa sarafu za fedha.
Na watu hao watakuwa na haki ya kuagiza kiwango cha pesa wanachohitaji.
Usiku huu wa mwezi uwe wa faida kwenu nyote.
Hongera.
Aishi maisha marefu Sultani.
Aishi maisha marefu Sultani.
Aishi maisha marefu Sultani.
Aishi maisha marefu Sultani.
Aishi maisha marefu Sultani.
Sultana, inaonekana kuwa umati umekubali kutoka moyoni
kila badiliko linalofanywa na Sultani Iltumish.
Ni nini mtu anaweza kufanya na moyo huu wa kijinga hata hivyo?
Hakuna haja ya kuusifu moyo huu sana.
Kwa sababu huwezi kujua wakati moyo huu unakupeleka juu
na wakati moyo huo huo unakupeleka kwa matatizo.
Nisamehe kwa ujasiri wangu, Sultana.
Lakini natumai kuwa hizo sarafu za fedha hazitafanya sarafu za dhahabu ziwe hafifu,
hizo sarafu za dhahabu ambazo zilitengenezwa
na marehemu mume wako Qutubuddin.
Haichukui muda mrefu kwa nyakati kubadilika, Adila.
Kulikuwa na wakati mume wangu Qutubuddin hakuweza kushindwa.
Na sasa leo? Leo nyakati ziko upande wa Sultani mpya, Iltumish.
Wakati ufalme unabadilika, nyuso pia zinabadilika.
Nitaenda kuangalia matayarisho ya sherehe ya Eid.
-Hujambo. -Sijambo.
Nilichokuwa ninasema ni kuwa unaweza kuja kukutana nami pia.
Mimi si msichana wa harimu, mimi ni mamako, Shamshad Begum.
Bila shaka. Tafadhali pokea salamu zangu.
Qutub mpendwa.
Inaonekana unapanga kusherehekea
sherehe ya Eid kwa adhama kuu. Sivyo?
Bila shaka, mama.
Nimekuwa nikingoja siku ya leo kwa miaka mingi.
Na sasa vile nimepata nafasi hii,
kuwa na Sultani wakati huu wa Eid baada ya miaka mingi,
ninawezaje kosa fursa hii?
Kwa sababu kwa miaka mingi amekuwa aidha anashughulika na vita ama Lahore.
Umesema ukweli.
Tukiangalia sherehe kwenye kasri hivi sasa,
nakumbuka wakati Qutubuddin alikuwa mamlakani.
Ni nini tatizo, mama?
Unaonekana kusumbuka kusikia jina la baba. Kila kitu kiko sawa?
Sina wasiwasi kuhusu jina la mume wangu, nina wasiwasi kuhusu kazi ya mume wako.
Haya ni mabadiliko ya aina gani, Qutub?
Mabadiliko ambayo yanafuta jina na sifa za babako.
Haya ni mabadiliko ya aina gani?
Ammi, huelewi.
Wewe tazama na uone.
Kwa sababu ya ukarimu wa Sultani,
jina la baba litaandikwa kwa dhabhabu kwa kurasa za historia.
Ili jina lake liandikwe kwa kurasa za historia,
Sultani Qutubuddin Aibak hamtengemei mtu yeyote kabisa.
Alikuwa Mfalme na siku zote atakuwa Mfalme.
Nyanya, Ammijaan.
Hujambo, mama.
Ammi, angalia hii.
Zawadi ya baba ya Eid.
Ona taraza. Imeagizwa kutoka Persia.
Na hizi lulu zimetoka Basra.
Kweli inapendeza.
Umefanya kazi nzuri sana, Shazia.
Kwa muda mfupi, umetengeneza rinda la kupendeza sana.
Ammi, angalia hivi vito.
Kazi ya umakini.
Inaonekana kama imetengenezwa na fundi stadi.
Binti mfalme Razia yuko wapi?
Razia hampendi babake kwamba hawezi kumsaidia Shazia kufanya kazi hii yote?
Hataki kumpatia babake zawadi?
Hata hivyo, pia mimi ni nani wa kuuliza?
Lazima anazunguka na baadhi ya watumishi.
Kwa kurandaranda katika barabara za Delhi, huyu msichana
ataleta aibu kwa kasri ya ufalme.
Adila.
Amrisha binti mfalme aje mbele yangu.
Unawaza kuhusu nini, Razia?
Kama mawazo ni ya ndani zaidi basi nia inakuwa dhaifu.
Unahisi hofu?
Hofu ni muhimu zaidi kwako kuliko upendo kwa babako?
bBinti mfalme, mbona umekuja hapa?
Watu walioletwa hapa huadhibiwa
na kurushwa mbele ya chui milia walio na njaa.
Binti mfalme tafadhali twende. Ninaogopa. sana
Pia mimi ninaogopa, Chanda.
Lakini lazima nitoe unywele mmoja wa chui milia kwa ajili ya babangu.
Unywele aa chui milia?
Hapana, binti mfalme, huwezi kufanya hilo.
Hapana Chanda, nitafanya kazi hii mwenyewe.
Waambie tu wafungue mlango.
Hapana, binti mfalme. Huyu chui milia ni anayekula watu.
Kwa kawaida ni mkali.
Hawezi kujisaidia kutokana na hali yake
na pia mimi siwezi kujisaidia kutona na tamaa yangu.
Sitatoka hapa hadi nipate ninachotaka.
Binti mfalme, tafadhali acha.
Binti mfalme.
Fungua mlango. Hii ni amri ya binti mfalme Razia.
Ni suala la unywele tu. Kwa hivyo tafadhali nipatie.
Unasemaje?
Kuwa mwangalifu, binti mfalme.
Kuwa mwangalifu, binti mfalme.
Mtu amuokoe binti mfalme.
Mungu wangu, kuwa na huruma.
Hashim, anza kufunga mlango.
Hashim, funga mlango haraka.
Binti mfalme, uko sawa, sivyo?
-Binti mfalme Razia. -Aishe maisha marefu binti mfalme.
-Binti mfalme Razia. -Aishe maisha marefu binti mfalme.
Msinisifu sana. Kweli nimekwepa leo.
Hata hivyo nilikuwa naogopa sana.
Hata mimi mwenyewe sijui jinsi nilivyofanya hilo.
Limefanyika tu.
Nilifunga macho yangu, na kutaja jina la Mungu,
nikaweka mguu wangu kichwani mwake na kuchukua nywele.
Shika hii. Sasa twenda.
Twende wapi sasa?
Tumepata nywele ya chui milia kwa sasa.
Sasa bado ninahitaji kumpelekea baba zawadi mbili zaidi.
Kidogo zaidi, tuzunguke kwa muda.
Nikitembea hata hatua moja zaidi, kwa hakika nitakufa sasa.
Binti mfalme, niambie mbona tumekuja kwa jangwa hili kutoka eneo la upweke?
Ule mti unaoona pale.
Nataka kuchukua jani kutoka mti huo nimpatie babangu.
Mungu wangu.
Hata hivyo kuna uhusiano gani kati ya babako na majani hayo?
Nitaleta hayo majani kwanza kisha nitakueleza.
Jamani! Binti mfalme Razia na matamanio yake.
Ni aidha yeye ama Mungu anajua kuyahusu.
Binti mfalme Razia, unaenda wapi?
Tulia tu na uje nami.
Binti mfalme, ninahisi uoga sana.
Kama kuna mtu atatutambua, kutakuwa na shida kubwa.
Na je Malkia akijua?
Atajua tu tukipatikana, sivyo?
Umeona duka la Nizamuddin?
Sijui, unaweza kuuliza mbele.
Nyinyi wafanyakazi, mnaelewa lugha ya kiboko tu?
Nitawachapa viboko hadi ngozi zenu zibambuke.
Nyinyi wajinga, ninazungumza lugha geni?
Toa huo ubao wa Nizamuddin na uweke ubao wa Rehmat badala yake.
Rehmat muuza zulia.
Hata mbwa wanaelewa vizuri kuwaliko.
Wewe msichana, unatazama nini hapa?
Kuna mchezo unaoigizwa hapa?
Ondoka hapa.
Toka.
Bwana, duka la hariri la Nizamuddin liko hapa?
Nini? Umesema nini, msichana?
Wewe ni kipofu? Mimi ndiye mmiliki wa duka hili.
Hakuna Nizamuddin anayeishi hapa. Alikufa kitambo.
Inawezekanaje?
Kwa nini? Sasa mtu anahitaji ruhusa ya kufa kutoka kwa watumwa?
Jamani, tokeni hapa.
Mungu, nitamalizaje zawadi ya babangu sasa?
Sikiza.
-Umekuja kumwona Mohammed Nizamuddin? -Ndiyo.
Nifuate.
Baada ya miaka mingi,
kuna mtu amekuja kuniona.
Hata hivyo ni nani anajisumbua kujua ikiwa
huyu fundi stadi anayezeeka ikiwa yuko hai ama amekufa?
Usiseme hivyo, mjomba.
Tunakushukuru sana.
Kama hungekuwepo, basi pengine mimi pia singekuwa hapa.
No comments yet. Be the first to leave one.