200 ensimmäistä riviä.
Unataka kujua kwa nini?
Yeye ni mtoa habari wetu.
Amepata kitu kutoka maisha yako ya nyuma.
Kurasa zinazoonyesha hadithi tofauti ya maisha yako.
Lakini mfalme mkuu, hii...
Unatoka Bhatinda, sivyo?
Huna familia wala marafiki.
Uliwapoteza wazazi wako ukiwa mtoto.
Wewe ni yatima.
Kama mhamiaji umezurura huku na kule.
Halafu ukaenda kwa muuaji Haji Jamal.
Aliyekufunza kupigana na kuua.
Kuuza dhamiri yako kwa shilingi chache.
Aliyekufunza kuwaua wasio na hatia.
Inaaminika,
kwamba katika dunia ya wauaji,
hakuna mpiganaji bora kukuliko.
Haya yote ni ukweli, mfalme mkuu.
Lakini niliacha hayo yote nyuma.
Unaweza kuwa umeacha siku zako za nyuma,
lakini kwa bahati mbaya, siku zako za nyuma hazijakuacha.
Na leo, nasimama mbele yako
na unasimama hapo ukiniangalia.
Razia ni muhimu sana kwangu.
Yeye ni kila kitu kwangu. Upendo wangu, majivuno yangu.
Baba yeyote angetaka binti yake awe na mtu ambaye,
ana furaha naye.
Anayehisi salama naye.
Anayeweza kumpatia maisha ya heshima.
Lakini mikono yako imejaa damu ya wasio na hatia, Mirza.
Nikijua haya yote, nawezaje kukupa mtoto wangu?
Natumai,
mepata majibu uliyokuwa unatafuta.
Sina mengine ya kusema.
Unaweza kuondoka.
Siwezi kutimiza matamanio yako.
Siwezi kuruhusu Razia aolewe nawe.
Baba yeyote angetaka binti yake kuwa na mtu
anayeweza kumpa maisha ya heshima.
Lakini mikono yako imejaa damu ya wasio na hatia, Mirza.
Dunia inakujua kama "Lakh Baksh."
Mkarimu anayetoa mamilioni.
Lakini najutia Sultani Iltumish,
umeniangusha.
Huna chochote cha kunipa?
Mfalme mkuu mwenye hekima kama wewe,
alihusika na siku zangu za nyuma?
Maisha niliyoacha nyuma,
umenikataa kwa sababu hiyo?
Nakuuliza Sultan Iltumish.
Siku zako za nyuma,
maisha yako ya nyuma,
hayana dosari?
Cha muhimu katika maisha, Sultani,
ni sisi ni nani leo.
Si tulikuwa nani zamani.
Umeingia kwa ruhusa ya nani?
Sultani...kuna damu kwenye mdomo wako...
Mirza...kifo kinanikaribia.
Nina muda mfupi sana.
Wakati wowote kinaweza kunichukua.
Sasa, labda utaelewa kwa nini nilifanya uamuzi huu.
Mirza.
Mirza, jaribu kunielewa.
Uamuzi wangu mbaya,
unaweza kuharibu maisha ya binti yangu.
Na iwapo kitu kitavunjika,
ni vigumu sana kukiunda.
Na pia, labda sitakuwa hapo
kurahisisha maisha.
Ninaweza kutoa ombi, Mfalme Mkuu?
Nataka kumjulisha Binti Mfalme Razia,
kwamba labda si jaaza yetu kuwa pamoja.
Lakini kwa kweli kulikuwa na kitu kati yetu
na sasa mwisho wetu ni tofauti
na njia pia.
Una moyo wa kujali.
Na sasa, unafaa
kuweka siri ugonjwa
huu wangu.
Hakuna anayefaa kujua
kwamba Sultani Iltumish
ana pumzi chache zilizobaki.
Sultani!
Hata Razia.
Nakuahidi, Sultani.
Siri hii itafichwa kwenye kifua cha Mirza.
Maisha yako yanapochukuliwa,
siwezi hata kukutakia
furaha na mafanikio.
Lakini, Mirza...
...nakutakia mema siku zote.
Hii ni ahadi yangu.
Razia...mtoto wangu!
Nisamehe, kama unaweza.
Ninajua,
kwamba utakuwa na huzuni mara tu utakaposikia haya.
Lakini nime...
nimefanya haya yote kwa faida yako, mtoto wangu.
Kwa faida yako.
Njoo. Njoo.
Unaona hali yangu?
Huyo Iltumish wako amenifilisisha.
Huyo mja Mirza anavaa nguo bora kuniliko.
Na haikusumbui?
Umevaa vizuri!
Naongea na wewe.
Sema kitu.
Hali yako sasa...
...niko katika hali mbaya zaidi.
Nimebaki na nguo mbili tu.
Na angalia watumwa hawa.
Hakuna anayetaka kuongea na mimi.
Na ni kwa sababu ya Razia.
Nikimalizana naye,
-dunia itatazama. -Hapana.
Usiseme chochote. Chochote.
Kila mara umeshindwa.
Lakini wakati huu, kumbuka, mama.
Kitu chochote kikienda vibaya,
hatutaweza kuimba na kucheza densi kupata pesa.
Ni suala la muda, bwana.
Acha wakati upite.
Hii ni nzuri,
kwa sababu ya Razia, mamlaka na umaarufu wote umeisha.
Hakuna atakayetushuku.
Sasa tunaweza kufanya mambo chinichini. Kufanya kinachohitajika kufanywa.
Umesema kweli, mama.
Lakini haya yote yatatokea lini?
Ili kutikisa misingi,
basi itafanyika tofali kwa tofali.
Wewe na mimi ni siafu
ambao wataharibu ufalme huu
na Mfalme Mkuu hatajua.
Kuwa na uvumilivu.
Mtu aliniambia,
baada ya uvumilivu huja starehe.
Fatima, inaonekana Mirza aliongea na babangu.
Lazima alimwambia kila kitu, sivyo?
Nitaaibika sana kwenda mbele ya baba.
Ni kweli. Watu hufanya mambo ya ajabu wakiwa wapenzi.
Kwanza enda uangalie kama Mirza aliongea au la.
Halafu unaweza tahayari.
Ndiyo. Wakati mwingine wewe pia huongea ukweli.
Nitaenda kwa Mirza na kumuuliza.
-Fatima! Ninaonekanaje? -Nini?
Binti Mfalme unaonekana sawa.
Uko sawa? Umezidi.
Ni Mirza yule yule.
Mmewahi kuacha kuangaliana? Ni nini mbaya sasa?
Fatima, huelewi.
Mahusiano yakibadilika,
mtazamo wako kwa mahusiano pia unabadilika.
Sasa...sasa nitakuwa mke wake.
Na...
Na atakuwa mume wangu.
Kwa hivyo si ni lazima niende mbele yake kwa tabia inayofaa?
Unaajabisha, Binti Mfalme! Tabia inayofaa?
Sasa enda. Enda.
Jiangalie ukiringa
baada ya kumuomba Sultani unioe.
Binti Mfalme.
Njoo hapa kwa muda. Njoo.
Ndiyo. Sasa niambie baba alisema nini?
-Uh...ni... -Sema haraka.
Mimi pia nashangaza. Baba lazima alikubali.
Sasa niambie ni lini anafikiria tuoane.
Hivi karibuni.
Hivi karibuni sana.
Maula wangu.
Maoni yako kuhusu Mirza ni gani, Sultani?
Yeye ni mzuri. Jasiri...
Na mwaminifu pia. Na jambo kubwa zaidi ni...
...wakati wa shida hata watu wetu watatuacha.
Lakini amekuwa na sisi.
Basi hujamkubali kwa Razia wetu?
Kwa sababu nina ndoto zingine kwa Razia.
Ni nini mbaya Mirza? Kwa nini unaonekana hivi?
Ninaongea kuhusu harusi na una huzuni.
Nani anajua kitachotokea baada ya harusi?
Ni nini mbaya, bwana. Kwa nini umehuzunika?
Kwani hunipendi?
Kwa kweli,
sikutaka kukwambia.
Lakini ulinilazimisha.
Na ninaweza kuuliza kwa nini unanificha mambo yanayohusika na ndoa yetu?
Kwa sababu,
Sultani Iltumish hakutaka.
Unamaanisha nini?
Inamaanisha, Binti Mfalme,
Sultani hakutaka kuzungumiza wazi.
Maoni yake ni, hadi harusi yetu itangazwe,
nisimwambie yeyote.
Hata wewe.
Oh!
Basi nimefanya makosa.
Nimefanya uvunje ahadi yako kwa Sultani.
Unaweza kuniadhibu unavyotaka lakini nisamehe kwa kosa hili.
Naapa, sitamwambia yeyote.
Hata sitamwambia baba.
No comments yet. Be the first to leave one.