Pierwsze 200 wierszy.
Ninaamini hadi uamuzi thabiti ufanywe,
utasimamia cheo cha waziri.
Maham Anga!
Nisamehe Mfalme.
Ninashukuru kwa heshima ambayo umenipa.
Lakini sitaki kuwa waziri.
Kama vile Khan Bahadur alisema, si vyema
kwa wanawake kuingilia masuala ya siasa.
Ninafurahia kukuhudumia nikiwa kwa harimu.
Nitavunja sheria hii.
Baada ya kuivunja, hakupaswi kuwa na tatizo lolote.
Kuna shida nyingi.
Mfalme, sitaki kuwa waziri.
Je, kuna mtu unayejua...
anayefaa kuwa kwa cheo hiki?
Punde tu jina la Shamshuddin litakapopendekezwa
kwa Ukumbi wa Mazungumzo ya Faragha.
nitatoa pendekezo na nyote mtaniunga mkono.
Hali ni mbaya sana. Huyo alikuwa Bahadur Khan.
Yeye ni adui yetu.
Ninajua.
Watu wote wanamuunga Bahadur Khan mkono.
Khan Aiya, Sultani Hussein Jalil, Mohammed Amin Dewana,
wote wanatupinga.
Itakuwaje Bahadur akiwapa habari?
Atawajulisha.
Tutafanya urafiki na maadui zetu
kwa vita hivi vya kisiasa.
Unataka kufanyeje?
Kitu...
...kitakachoshtua maadui wetu katika Ukumbi wa Mazungumzo ya Faragha.
Maham Anga alijua kuwa Bahadur Khan alisikia mazungumzo yake.
Shangazi hebu niambie. Una maoni yapi?
Maham Anga.
Bahadur Khan.
Baada ya Khan-e-Khan,
yeye pekee ndiye anajua kila kitu kuhusu vita.
Pia anafahamu maeneo ya mipaka vizuri sana.
Maham Anga alifanya kile ambacho watu hawakudhani.
Kwa kumteua Bahadur Khan kuchukua nafasi ya Bairam Khan,
aliungwa mkono na maadui wake.
Vizuri sana.
Hongera.
Bahadur Khan na wafuasi wake
walikubali uwezo wa Maham Anga.
Bahadur Khan alipata cheo cha Bairam Khan.
Lakini alipata cheo pekee.
Maham Anga ndiye alikuwa na mamlaka ya cheo hicho.
Maham Anga!
Adham Khan, mwana wa Maham Anga
alijinufaisha kwa kutumia mamlaka ya mamake.
Baada ya kupoteza mumewe Ibrahim, angali mchanga,
Bakshi Banu hangeacha kulia.
Alienda Agra kukutana na kakake Jalal.
Kaka.
Kaka, nilifanya dhambi ipi?
Mbona jambo hili lilinitendekea?
Ruqaiya, mpeleke kwa chumba chake.
Kuanzia leo, utaishi na sisi, chini ya ulinzi wangu.
Mama, jambo lililomtendekea Bakshi Banu halikuwa sahihi.
Ibrahim alikuwa mchanga sana.
Dadangu ataishije maisha yake yote akiwa peke yake?
Bakshi Banu akiolewa mara ya pili
na mwanangu Adham, hilo litakuwa jambo zuri sana.
Leo mimi ni yaya ya Jalal lakini baada ya ndoa hii,
nitakuwa jamaa yake.
Baada ya ndoa hii, maafisa wote
watainama mbele yangu.
Jalal ukiniruhusu, nina wazo ambalo ningependa kusema.
Shangazi nimekwambia mara nyingi.
Huhitaji kuniomba ruhusa ili uniambie kitu chochote.
Niambie.
Miezi sita imepita tangu Ibrahim afe.
Wakati wa kuomboleza umepita.
Mbona tusimwoze Bakshi Banu tena?
Ninakubaliana na wewe kabisa.
Nitafanya uamuzi kuhusu jambo hili, haraka iwezekanavyo.
Uamuzi unapaswa kumfaa Adham.
Jalal akikubali posa ya Adham ya kumwoa Bakshi Banu,
si harimu pekee itatii amri za Maham,
bali ni nchi nzima.
Sita. Ni sita.
Vizuri!
Angalia kaka. Umepoteza kibaraka kingine.
Kwa uhakika utashindwa.
Dada, si vyema kuota mchana.
Acha nicheze kwanza, kisha tutaongea.
Padri wa kifalme atakuja kesho.
Jodha ataolewa baada ya siku chache.
Baada ya ndoa yake, tutabaki na kumbukumbu zake pekee.
Kaka zake wanajaribu kutengeneza kumbukumbu hizo.
Angalia, wameacha kazi zao zote
na wanajaribu kumfurahisha Jodha.
Kwa kufanya hivyo, wakati ni sawa kwa kila mtu.
Lakini ninafikiri wakati huenda haraka,
kwa nyumba zilizo na mabinti.
Sikujua Jodha wetu akikua.
Tumeshinda! Tumeshinda!
Kaka, hujafanya jambo sahihi.
Umeshindwa kimakusudi ili unifurahishe, sivyo?
Jodha, ushinde mdogo hauwezi kukilinganishwa na furaha yako.
Nitataka kaka zangu washinde daima kwa mchezo au kwa vita.
Hata miungu wanaabudu uhusiano huu
Maombi yako yakiwa nasi, ni nani anaweza kutushinda?
Upendo wa kaka na dada
Maham Anga anacheza mchezo
kwa kutumia binadamu kama vibaraka.
Kwa mara ya kwanza katika Ukumbi wa Mazungumzo ya Faragha wa Ufalme wa Mughal,
mwanamke amepaza sauti yake.
Ninahitaji kuwa makini kuhusu Maham Anga.
Malkia, unapata wasiwasi bure.
Wewe ni Malkia wa Uhindi.
Lakini Mfalme amempatia hadhi ya mamake.
Kumbuka kuwa,
kwa mwanamume yeyote, mama ni muhimu zaidi kuliko mke wake.
Ninaona hadhi ya Maham Anga
na ujanja wake unakua siku baada ya siku.
Maham Anga.
Habari yako Malkia.
Umeniita?
Kuja. Kuja.
Nimetamani kucheza sataranji na wewe baada ya muda mrefu.
Na hatukumaliza mchezo wa juzi.
Mbona tusiumalize sasa hivi?
Utakavyo Malkia.
Maham Anga!
Malkia, acha nikukumbushe kuwa ni zamu yako ya kucheza.
Ninakumbuka.
Wakati uliopita, ulicheza mchezo
ulionipa muda wa kufikiria vile ambavyo nitalipiza kisasi.
Huwa unacheza vizuri sana.
Kumradhi Malkia. Sijakuelewa.
Khan Bahadur alikuwa anakupinga, sivyo?
Nimesikia kuwa amekuwa kibaraka wako.
Nguvu zako zinaongezeka.
Malkia, ninataka kuongeza nguvu za ufalme wa Mughal pekee.
Ili ufalme uwe na nguvu zaidi,
ni lazima ushinde wapinzani wako.
Iwe kwa mchezo wa sataranji au wa siasa,
ni vyema kuchunga mipaka yako.
Malkia, ninajua mipaka yangu.
Lakini unapanua mipaka kwa ajili ya mwanako.
Khan Adham, ni kaka mkubwa wa Jalal.
Khan Adham akiwa maarufu,
Mfalme pia atapata umaarufu.
Maham Anga!
Umeshindwa Malkia.
Umenishinda haraka sana.
Ninafikiri una haraka ya kumaliza mchezo.
Malkia, sikuwa na haraka. Ni wewe ulikuwa na haraka.
Umeshinda Malkia wa Uhindi.
Malkia, huu ni mchezo tu.
Lakini niamini kuwa siwezi taka mtu yeyote ashinde Malkia.
Jalal huniita mama.
Ninakuahidi kuwa nitakuwa mwaminifu kwa Jalal na mkewe kwa maisha yangu yote.
Leo ninakuambia hivi.
Kesho historia itazungumzia uaminifu wangu.
Niruhusu niende.
Maham Anga alikuwa anashinda kila mtu kwa werevu wake.
Na mwanake Adham Khan alikuwa anatumia wakati wake
kujifurahisha baada ya Bairam Khan kuondoka.
Bwana.
Bwana, kuna habari muhimu.
Bwana, habari hizo ni kuhusu Bairam Khan.
Niambie.
Nimepata habari kuwa Bairam Khan amefika Gujarat.
Na ametafutiwa nyumba huko Patan.
Siwezi kumwamini Bairam Khan. Anaweza kurudi wakati wowote kutoka Mecca.
Hilo likifanyika,
sitaweza kutimiza malengo yangu.
Fanya jambo moja.
Tuma ujumbe kwa Pathan Mubarak Lohani.
Mfalme Padmabhan na Rudrabhan wanawasili.
Mtukufu, padri wa kifalme, nyote mmekaribishwa Amer.
Kwa niaba ya Bhanpur, tafadhali kubalini zawadi hizi za Binti Mfalme Jodha.
Mfalme, nimeamua tarehe yenye heri ya kufunga ndoa hii.
Tarehe yenye heri ya kufunga harusi ya
Binti Mfalme Jodha na Mwana Mfalmen Suryabhan
ni mwezi huu wakati wa mwezi mpevu.
Nilikuwa ninataka kukwambia kitu.
Ndiyo, Mainavati. Niambie.
Nilikuwa nimeapa kuwa punde tu tarehe ya harusi ya Jodha ikipangwa,
ningetolea Kali, mungu wa kike dhabihu hekaluni.
Na familia yangu yote itahudhuria.
Nini kinaweza kuwa kizuri kuliko Jodha kupata baraka za mungu wa kike
katika maisha yake mapya?
Hatupaswi kuchelewesha ibada hii.
Tutaenda huko leo jioni.
Hapa ni Ajmer na hapa ni Mewat. Katikati yao ni Amer.
Kundi moja la wanajeshi litatoka Ajmer na hilo lingine litatoka Mewat.
Na Amer itanaswa katikati ya vikundi hivyo.
Sharifuddin, kumbuka kuwa haitakuwa rahisi kushinda Amer.
Ngome ya Amer ni imara sana.
Jambo la pili, kuna njia za siri huko Amer,
zinazopatikana hapa, hapa na hapa.
Kwanza, itabidi tuweke wanajeshi wetu hapo
ili wasipate fursa ya kutoroka.
Watashinikizwa.
Tutaweza kupata ushindi haraka
bila kumwaga damu nyingi.
No comments yet. Be the first to leave one.