Pierwsze 200 wierszy.
Hujambo, mama.
Sijambo, Bi Salima.
Nilitaka kukutana nawe. Tafadhali, keti.
Nilitaka kujua kama umepiga hatua yoyote.
Je, ulipata kidokezo chochote kuwa Benazir ni msichana mwenye sumu?
Hapana, mama. Sijamuona Benazir akifanya kitu chochote kama hicho,
kinachoweza kunifanya nimshuku.
Lakini Bi Jodha ameshuhudia.
Sasa amemtenga Benazir kutoka kwa Mfalme.
Namna gani?
Mama, ilifanyika kuwa...
Mama, unaenda wapi?
Kujua ukweli kutoka kwa Benazir.
Kabla ya harusi hii kufanyika,
ni muhimu kukamilisha suala hili.
Bi Jodha anashughulikia pia.
Sidhani mtu yeyote anapaswa kuingilia suala hili.
Kwa nini?
Kwa kuwa nimeelewa kwamba,
Bi Jodha anampenda Mfalme.
Anafanya jambo hili kwa sababu hiyo hiyo.
Nataka Mfalme ajue...
kuwa Bi Jodha anajaribu kuokoa maisha yake.
Bi Salima, una nguvu kiasi gani?
Mke siku zote anamchukia mke wa pili wa mume wake.
Na wewe una...
Mtu humchukia mke wa pili wa mume wake,
lakini si dadake.
Bi Jodha ananichukulia kama dadake.
Na sikuwahi hisi...
kuwa Bi Jodha ananionea wivu au anamwonea Bi Ruqaiya.
Sawa. Kama unasema hivyo, basi nitafanya unavyosema.
Kwa neema ya Mungu mambo yatatokea unavyofikiria.
Amina.
Jodha, ulimpaka Mfalme dawa ile?
Jodha, nini kilifanyika? Sema kitu.
Nilikuwa nimeenda lakini...
Lakini nini?
Lakini Bi Ruqaiya hakuniruhusu nipake dawa hiyo.
Isitoshe, aliniamrisha niondoke.
Mfalme hata hakumzuia asinifanyie hivyo.
Angekuzuia kwa nini? Umemjeruhi.
Hapana, Moti.
Kama ni hivyo, basi ni kwa nini unaenda kwa Mfalme mara kwa mara?
Kwa nini unahuzunika, unafikiri kuwa wewe ndiye mkosaji?
Wakati Mfalme anakukasirikia kwa nini unamtembelea?
Ni sawa. Acha Mfalme akasirike.
Lakini simkasirikii.
Sawa. Mfalme anamuoa Benazir.
Na humkasirikii.
Moti, haya yametosha.
Licha ya kuwa unajua kila kitu, kwa nini unaniongezea machungu?
Unataka kusikia nini?
Kwamba nina wasiwasi kuhusu Mfalme?
Naam, ndiyo, nina wasiwasi kuhusu Mfalme.
Lakini kama mume ametekwa kwa mpango wa msichana mwenye sumu...
basi ni wajibu wa mke wake kumlinda.
Chochote ninachofanya ni wajibu wangu.
Mapenzi ni mazuri.
Wote wawili wanasumbuliwa na jambo moja.
Lakini hawakubali hilo.
Husemi hilo wala Mfalme hasemi.
Unasumbuka kama anavyosumbuka pia.
Bi Ruqaiya.
Je, uko salama?
Nasikia kwamba umekasirika na huli chakula chako.
Hoshiyar aliniambia kuwa bado hujala tangu asubuhi.
Hata mpishi aliniambia kuwa hukula kifunguakinywa au chakula chochote.
Kuna nini, Bi Ruqaiya?
Sihisi kula kitu chochote.
Kweli? Huhisi kula.
Una afya tayari, bibiye.
Ukitoa hasira yako kwa chakula,
basi utakapokwenda kuwinda wakati ujao,
utabebwa na ule upepo mkubwa!
Nitakwenda kuwinda wakati Bi Jodha ataachana na Jalal.
Anatafuta kijisababu cha kuwa pamoja na Jalal kila wakati.
Nimeelewa sasa. Hukasirikii chakula.
Unamkasirikia Bi Jodha.
Angalau ni vyema kujua kuwa hukasirikii chakula.
Bibiye, si kosa lake.
Usimkasirikie. Nilimuwita.
Hii hapa.
Kula matunda.
Bi Ruqaiya, kula matunda tafadhali.
Sikiliza, sitaki rafiki yangu awe mdhaifu...
akiwa anapigana dhidi ya Bi Jodha.
Kula.
Maham Anga.
Sijamuona mwanamke asiye na aibu na mkaidi kama yeye.
Jalal hata hamtambui.
Lakini anaendelea kuenda kwa Jalal.
Sikiliza haya! Wakati huu alimtafutia mfalme dawa ya kupaka.
Ili kuonyesha watu wote kwamba hana hatia.
Kwamba anamjali Jalal zaidi.
-Je, ni hivyo? -Ndiyo.
Lakini nilimuonyesha Bi Jodha nafasi yake.
Nilichukua dawa ya kupaka kutoka kwake na kumuamrisha aondoke.
Kisha nikapaka dawa hiyo kwa jeraha la Jalal.
Nini?
Bi Ruqaiya, ulifanya nini?
Ulimsaidia Bi Jodha.
Ulifanya kosa kubwa sana.
Ulipaka dawa aliyoleta kwa jeraha la Jalal.
Usiniangalie namna hii.
Fikiri kuhusu hilo.
Dawa ya kupaka ambayo Bi Jodha alileta ilipakwa kwa jeraha la Jalal?
Bi Jodha mwerevu alikufanya ufanye kazi yake.
Alimletea Jalal dawa.
Na alikujeruhi.
Alifanya kazi yake kwa werevu.
Alipata huruma ya Jalal pia.
Maham Anga, acha kunihuzunisha tena.
Kama una suluhisho lolote basi niambie.
Au unaweza kuondoka kutoka hapa.
Bi Ruqaiya, pole.
Sina dawa ya kupaka kwa majeraha yako.
Lakini nina suluhisho kwa tatizo lako.
Hiyo ni nini?
Mfukuze Bi Jodha kutoka Agra.
Mtenge Bi Jodha na Jalal.
Jalal atamsahau Bi Jodha pindi tu utakavyofanya hivyo.
Uchawi?
Huu ni ujinga.
Si ujinga.
Fungua akili yako. Angalia na macho yako!
Kila kitu kinafanyika mbele ya macho yako.
Benazir alilaumiwa kuwa ana sumu, jambo ambalo halikuwa kweli.
Lakini Mfalme hakumwadhibu Bi Jodha aliyemlaumu kwa uongo.
Ni nini kama sio uchawi?
Dadake Bi Jodha, Shivani...
alitoroka na mpenzi wake siku ya harusi yake.
Alimdanganya Mirza Hakim, mtu aliyependwa zaidi na Jalal.
Lakini badala ya kumwadhibu mfalme Bharmal,
aliachiliwa kwa heshima kabisa.
Unaita hiyo nini? Si huo ni ushahidi wa uchawi wake?
Mungu wangu!
Wewe ni malkia mwerevu.
Ulisema kwamba unacheza na akili ya Jalal.
Shinikiza akili hiyo na ujue uchawi wa Bi Jodha,
ulioko akilini mwa Jalal.
Tafadhali fanya jambo, Bi Ruqaiya.
Kwa ajili yako.
Vunja uchawi wa Jodha.
Kwaheri!
Sili miboga yoyote.
Nataka dawa yangu.
Tikiti maji hii si yako.
Lakini kile kilichonacho kinaweza kukuvutia.
Unasema nini?
Ina nini ambacho kinaweza kunivutia?
Sasa, niambie?
Hii ni nini?
Ramani.
Ya nini?
Gereza ile.
Mfuasi wa zamani wa Abul Mali ametuma ujumbe huu.
Ni wakati wa kumtoa Abul Mali gerezani.
Nakutumia ramani ya gereza hilo.
Nataka kukwambia baadhi ya mambo muhimu zaidi.
Tukutane sokoni mara moja.
Hiyo ni nzuri.
Hatupaswi kupoteza muda wowote.
Tutakapojua jinsi ya kumfikia Abul Mali kutoka kwa Kamal Khan,
basi nitamwachilia huru.
Tutalazimika kumaliza kazi hiyo kabla mtu ajue.
Benazir, tutaendaje huko?
Kama watu watakutambua mara nyingine, nini kitafanyika?
Itakuwaje kama watakushambulia?
Wakati huu watu hawatanitambua.
Nitavaa hili. Sikiliza.
Hatuendi pamoja wakati huu.
Inaweza kuwa hatari kwetu kuenda huko pamoja.
Bi Jodha, umefikiria kuhusu hatua yako inayofuata?
Sijui hatua ya Benazir inayofuata.
Nitalazimika kumfuatilia kwa makini kila wakati.
Nitapata suluhisho kulingana na tatizo litakalojitokeza.
Je, hilo litasaidia kwa kweli?
Sijui.
Lakini, angalau nitajua...
kile ambacho Benazir anafanya na kule anakoenda.
Sina chaguo lolote kando na hii.
Lakini Bi Jodha, Benazir ni mwerevu sana.
Itakuwaje kama atajaribu kutudanganya?
Basi, tutapaswa kuwa werevu sana.
Natumai, kutokana na hali hiyo,
Mfalme ana ulinzi mkali.
Katika hali hii, Benazir atakosea.
Ni hivyo. Tutatumia kosa hilo kama silaha yetu.
Jodha, kuja hapa.
Angalia, Benazir anakwenda mahali.
Ndiyo. Anaonekana kuwa na haraka.
Kwa nini amevaa nguo za mtumishi?
Ili mtu yeyote asimtambue.
Inamaanisha...
-Atachukua hatua yake inayofuata. -Atachukua hatua yake inayofuata.
Bi Salima, fanya haraka. Lazim tumfuate Benazir.
Lakini Bi Jodha, itakuwaje kama hiyo ni hatari?
Ndiyo. Hii haitakuwa rahisi.
Fanya hivi. Baki.
No comments yet. Be the first to leave one.