Pierwsze 200 wierszy.
Ndilo hili toleo.
Nilikuwa nikitoka hekaluni.
Nilikuona hapa, kwa hivyo nikaja kukupa toleo.
Umenikasirikia mimi si toleo.
Lichukue.
Sasa, niambie kile ambacho hukupenda jana.
Ulifedhehesha roho yangu kimyakimya.
Unamaanisha nini?
Je, nahitaji kukuelezea hili?
Unafikiriaje?
Sitaelewa maana
ya kunizawadia susu ile?
Kwa kunyamaza, umenidhihaki
kwamba nimeshindwa kuupa Ufalme wa Moghul mrithi.
Kinaya iliyoje!
Mamako ananizawadi mkufu wa mababu
kwa ajili ya susu na unachukulia
susu hiyo kama kushindwa kwako?
Shida ni mtazamo wako si susu yangu.
Unamaanisha nini?
Je, mtazamo wangu si sahihi?
Ndiyo, bila shaka.
Ulichukulia matakwa yangu ya heri kama dhihaka.
Na kwa kweli mchoro wa Benazir
haukuwa unastahili zawadi.
Picha yako kamwe haiwezi kuuzika sokoni.
Lakini bado ulimzawadia.
Kwa hivyo, mtazamo wako si sahihi.
Basi, kubali kwamba umeumia kwa sababu nampa
Benazir umuhimu zaidi kukuliko.
Si mimi, lakini kila mtu anaongea.
Kwamba kwa muda mfupi sana,
Benazir amekuwa muhimu sana kwako.
Jodha Begum, mimi ni mfalme mkuu.
Sihitaji kuelezea kila mtu
kile ninachokifanya au vitu ninavyovipenda na vile sivipendi.
Na kwa kweli, mtazamo wako si sahihi.
Nilikuamini. Nilikwenda kinyume na kila mtu kwa ajili yako.
Na ulifanya nini kama malipo?
Ulinikosea heshima sokoni.
Ulishuku uume wangu.
Si wa mfalme mkuu tu lakini pia umemfedhehesha mume.
Kwa kuwa mume wako, nina kila haki kwako.
Lakini hapana.
Kabla ya kuzungumzia mtazamo wangu,
ni bora ufikirie wako.
Hiyo itakuwa afadhali.
Mtukufu, wewe...
Moti, ulikuwa wapi?
Nilikuwa nikifanya matayarisho yako ya kuoga.
Kule nilikutana na Bela.
Yule anayempa kila mtu bidhaa za urembo.
Alikuwa akigawa bidhaa mpya kule.
Alisema kwamba bidhaa hii itang'arisha ngozi.
Na urembo wa mtu utang'aa.
Wakati wa majira ya baridi, bidhaa yenye mafuta ya lozi inanufaisha sana.
Kila mtu alikuwa akiichukua.
Kweli? Iko wapi?
Sikuileta. Nilimwambia kwamba Jodha Begum
hahitaji bidhaa yoyote kwa ajili ya urembo wake.
Yeye ni mrembo tayari.
Mwongo. Jana ulikuwa ukimsifu Benazir.
Sawa, niambie kitu kimoja, Moti.
Je, kila mtu anasifu urembo wa Benazir?
Ndiyo. Yeye ni mrembo.
Lakini urembo tu hautasaidia.
Ndiyo maana ulipata mkufu wa mababu na si yeye.
Ndiyo, hiyo ni kweli.
Kama ni hivyo, basi kwa nini hujafurahi?
Lakini almasi ambayo Mtukufu alimpa...
Sikiza, nadhani una wasiwasi sana kuhusu Benazir.
Hapana, sina tatizo na Benazir.
Nafikiria maneno ya Mtukufu.
Maneno yake yaliniacha na fikira.
Nadhani mtazamo wangu kwake sio sahihi kwake.
Anazungumza kwa uchungu.
Lakini maneno yake yanaweza yakawa kweli.
Inawezekana kuwa kutoka upande wangu,
kutoka kwa tabia yangu, amepokea
vidokezo visivyofaa.
Kwa hivyo, si uongee naye wazi?
Ndiyo, ninataka pia
kuomba msamaha kwa ufidhuli wangu.
Lakini haongei nami.
Kwa sababu hujaribu.
Unamfikiria sana Benazir
na si Mtukufu.
Badilisha fikira zako, utapata fursa bila shaka.
Ndiyo, labda unasema ukweli, Moti.
Napaswa kumfikiria Mtukufu na si Benazir.
Jamani, harakisha, ninachelewa.
Tahadhari, babangu ametuma shali hii kutoka Amer.
Utachafuka ukianguka chini.
Sijui hayo yote. Harakisha.
Rahim, tembea polepole, unakimbia.
Wewe ni mkubwa kuniliko. Huwezi kutembea na mtoto?
Kimbia unishike.
Rahim.
-Hujambo, Mtukufu. -Hujambo.
Nilidhani uliniita hapa peke yangu.
Mimi pia sikujua. Tafadhali cheza naye.
Nitaondoka.
Siimama! Nina kazi nanyi wawili.
Kwa nini? Hiyo ni kazi gani, Rahim?
Nataka kurusha kishada.
Nyinyi wawili mnajua sanaa hii.
Ndiyo maana niliwaita.
Sijarusha kishada kwa siku nyingi.
Lakini kuna baridi sana, Rahim.
Tukikaa nje katika hali hii ya anga, tunaweza kupata homa.
Kwa nini mimi nipate homa
kama Mtukufu hapati? Sivyo, Mtukufu?
Na nikisema hata mimi ninahisi baridi?
Mtu yeyote anaweza kupata homa, Rahim.
Na ukigonjeka, Salima Begum atanikasirikia
kwamba sikukutunza.
Nimeelewa. Wote wawili hamtaki kurusha kishada, sivyo?
Usijali.
Hali ya anga itabadilika siku moja.
Wakati huo lazima urushe kishada na mimi.
-Unaniahidi? -Ndiyo.
Pole kwa kukusumbua, Mtukufu.
Rahim, mwanangu, Salima Begum anakuita.
Ndiyo, yeye hunitafuta kila wakati.
Hata hivyo, kuna baridi sana kwa kweli, sivyo?
Ndiyo maana niliagiza shali hii kutoka Amer.
Ukoje?
Kweli, ni nzuri sana. Rangi nzuri.
Utatoa joto wakati wa baridi.
Je, unaipenda?
Ndiyo, bila shaka.
Kwa hivyo, ichukue.
Asante kwamba umeipenda.
Kwa kweli nafaa kukushukuru.
Nilikuwa nikishangaa nifanye nini,
kumwokoa Benazir kutokana na baridi.
Nilikuwa nikifikiria kumwagizia mharuma unaopendeza hivi.
Na ona, umeuleta.
Hii ni zawadi nzuri sana kwa Benazir.
Mtukufu anapenda bustani hii sana, sivyo?
Ndiyo, nilisikia kwamba Mtukufu
anakaa hapa kwa muda mrefu sana.
Unafanya nini?
Kwa nini umemzuia?
Je, humjui?
Yeye ni mpendwa wa Mtukufu.
Mtukufu amempa cheo cha Kohinoor.
Pole kwa tabia isiyofaa ya walinzi wetu.
Nitakupitisha njia ile ingine.
Walinzi watakupeleka na vitu vyako.
Mimi ni bingwa wa kutunza vitu vyangu na kazi yangu.
Kazi yangu ni kumlinda bibi wangu na kuwa naye.
Sawa. Wewe pia njoo.
Kama ni sawa, nikwambie jambo?
Wewe ni mrembo sana.
Najua. Niambie jambo jipya.
Sawa. Acha nikwambie kuhusu hisia zangu.
Nimekuwa kichaa tangu nikuone.
Watu huhisi hivyo baada ya kuniona.
Lakini hali yangu ni tofauti kidogo.
Ninakufikiria kila wakati.
Nisaidie. Kaa nami jioni moja.
Hutajuta kwa ajili ya jioni hiyo.
Utajuta nikimwambia Mtukufu
jinsi ambavyo ulijibeba kwa mgeni wake maalum.
Na kwamba uliniomba nikae nawe jioni moja.
Mbona unaongea naye?
Anadhani anaweza kutumia cheo chake.
Nadhani hapendi maisha yake.
Acha tumlalamikie Mtukufu kukuhusu.
Wewe. Kaa mbali nami.
Jina lake ni Zakira.
Kuwa na tabia njema.
Usipuuze maumbile yake.
Anajua kutunza urembo wangu vizuri sana.
Na utajua nguvu yangu hivi karibuni
wakati nitakapokutana na Mtukufu.
Umekasirika.
Unajua kwamba mtu yeyote anaweza kupendezwa na urembo wako.
Kwa hivyo, mimi pia ni mmoja wao.
Hakuna haja ya kwenda kwa Mtukufu.
Nichukulie kama shabiki wako kichaa na unisamehe.
Naapa kuanzia sasa, sitakusumbua.
Lakini maliza jambo hili hapa.
-Tafadhali nisamehe. -Umefanya kosa kubwa.
Lakini uliweza kujua mipaka yako na hadhi yako haraka sana.
Kwa hivyo, enda. Nimekusamehe.
Ungelalamika kumhusu kwa Mtukufu.
Hapana, Zakira.
Nimekuja hapa kutimiza lengo langu si kupata maadui.
Na maskini jamaa hajakosea.
Urembo wangu unamwathiri mtu yeyote.
Sasa nahitaji kumpumbaza Jalal tu.
Javeda!
Mama, naonekanaje?
Huamini kwamba hata mimi ninapendeza sana, sivyo?
Nimejua hilo kila wakati.
Mimi pia ninaweza kupendeza kama Benazir.
Javeda, hutarogwa
ukijipamba kiasi hicho?
No comments yet. Be the first to leave one.