Jodha Akbar

Jodha Akbar

Pobierz napisy Swahili

Informacje o wydaniu

Jodha Akbar 2013 Episode 041-050 Swahili
Komentarz od kikywebsite

Tagi

other
Opublikowano: 2019-05-19
Pobrania: 25
Dla niesłyszących: No

Podgląd napisów Swahili

Pierwsze 200 wierszy.

Kwa baraka za mwenyezi Mungu na ujasiri wako...

...hili tukio mbaya liliepukika, mfalme.

Kama lolote mbaya lingetokea,

...jina la Amer lingeharibika.

Mbona una hofu kwa sababu ya tukio ambalo halikufanyika, mfalme?

Bwana, daktari wa mifugo alisema kuwa Hawai alitiliwa dawa

ndiposa akasababisha vurumai hiyo.

Nafahamu hilo, Adgha.

Najua kuwa mshambulizi alifahamu kuhusu uhusiano

kati yangu na Hawai.

Alijua kuwa chochote kingemkumba Hawai,

ningeenda kumsaidia.

Hivyo, maisha yangu yangekuwa hatarini.

Ilikuwa njama nzuri, lakini, iliepukika kwa uwezo wangu.

Adui alikuwa nani?

Anaweza kuwa yeyote.

Lakini sasa lazima tuwe macho, mkuu.

Inamaanisha kuwa nafaa kuishi kwa woga.

Adgha, mimi ni mfalme.

Nikitiwa hofu na visa vidogo kama hivyo, nitatawala ufalme mpana wa India vipi?

Adgha, nikiogopa, adui yangu atashinda.

Hivyo ndivyo adui hufanya.

Ananishambulia akitumai kuwa nitaogopa.

Nikiogopa, atashinda.

Lakini nikiishi bila woga, atashtuka.

-Lakini bwana... -Adgha!

Hii si mara ya kwanza nimeshambuliwa.

Nimeshambuliwa mara nyingi hapo awali

na litafanyika tena siku zijazo kwa kuwa mimi ni mfalme.

Lakini nitafanya nilichokuja kufanya bila woga.

Nitahakikisha kuwa Sukanya anafunga ndoa.

Mfalme, nimekuzidi kwa umri,

na bado najifunza mengi kwako.

Unaweza kufanya chochote utakacho,

lakini mimi pia nitatimiza jukumu langu.

Kwa sababu nina wadhfa, usalama wako ni jukumu langu.

Nitautekeleza.

Nitafanya msako kikamilifu ili kumpata

aliyefanya hii njama.

Nakuahidi.

Amer ni ufalme wako, mfalme.

Unafahamu unachopaswa kufanya.

Siwezi kukwambia jinsi ya kutawala.

Wewe unafahamu vizuri.

Lakini nikwambie kitu mfalme wangu?

Nina wasiwasi sana kuhusu Hawai, kuliko kuhusu mshambulizi.

Leo hii, huyo mnyama anahisi maumivu kwa sababu yangu.

Nisamehe, malkia.

Jalal ameshambuliwa.

Kunyamaza sasa hivi, kutaashiria woga.

Wakati mwingine kunyamaza ndilo jambo la busara, Maham.

Hata mimi nafahamu kuwa ufalme wa Mughal sio wa watu waoga.

Lakini hali ni tofauti.

Harusi ya Sukanya iko hatarini.

Malkia, una hofu kuhusu harusi ya Sukanya.

Huna wasiwasi kumhusu mwanao, Jalal?

Nakubali kuwa umemlea Jalal, Maham.

Lakini mimi nilimzaa Jalal.

Yeye ni nyama na damu yangu.

Namjali Jalal unavyomjali.

Lakini wakati mwingine unapaswa kusikiza akili yako, si moyo wako.

Adui anaweza kutoka Amer au Agra pia.

Umesahau kuwa Jalal hakuwa

amefika Amer aliposhambuliwa?

Mtaalamu wa mitishamba kutoka Gwalior alizuiliwa kuja

ili hali ya Jalal asiimarike.

Watu wetu wanajua vizuri kuliko watu wa Amer,

jinsi Jalal anampenda Hawai.

Mshambulizi anaweza kuwa yeyote kati yetu.

Jalal anaelewa hili vizuri sana.

Ndiyo sababu yuko kimya.

Katika uamuzi wowote ambao atachukua, nitamuunga mkono.

Samahani, malkia.

Nampenda mwanao, Jalal.

Ndiyo sababu mawazo kama hayo yalinijia. Kisha nikayasema hayo mawazo kwa sauti.

Nisamehe.

Maham, sime na maneno yanapaswa kutumika vizuri.

Vinginevyo, yatasababisha uharibifu.

Wewe ni mwamuzi katika ufalme.

Kwa sasa, fikiri kuhusu kutumia akili yako na sio moyo wako.

Nitafanya utakavyo.

Kwaheri.

Fanya chochote kile, umlete yule

ambaye amenipangia hila hii.

Lazima nimpeleke mbele ye mfalme.

Sielewi jinsi ya kukueleza hili.

Mbona huathiriwi na chochote?

Kwa sababu sitaki ushauri wako.

Wewe sio kiongozi wangu na sikutegemei.

Usisahau kuwa tuko kwenye mashua moja.

Hiyo mashua ikizama, sote tutapata hasara.

Sitastahimili hilo.

Umeona? Ulikosa lengo lako.

Ukikosa kwa mara ya pili, inamaanisha

mfalme atakuwa macho.

Sio mara mbili. Nitajaribu mara elfu moja.

Kazi yangu ni kuvamia, ilhali yake ni kutoroka.

Atatoroka kwa muda gani?

Siku moja atafanya kosa.

Lazima Jalal pia anawaza hilo.

Siku moja, utafanya kosa.

Halafu nini kitatendeka?

Jalal amekuwa makini sasa.

Tukifanya kosa moja tu, tutapoteza.

Nilifanya njama nzuri.

Hawai aliharibu mpango wote.

Anampenda Jalal sana.

Hivyo ndivyo ilivyo.

Ulijua Hawai anampenda Jalal sana,

lakini bado ukamchagua!

Nilikukutaza mara kwa mara.

Adham, wewe huwezi kabisa kubuni njama zozote.

Huna uwezo wa kuwa mfalme.

Angalau najaribu mara kwa mara.

Wewe hata huwezi kufanya hilo.

Huwa unasubiri tu kupata bahati.

Ninaamini katika kutengeneza hali stahifu.

Kuna wakati mwafaka kwa hilo pia, Adham.

Naam, nasubiri huo wakati.

Shambulizi linaweza kukawia kutekelezwa, lakini lisikose kufaulu.

Wale ambao husubiri wakati,

husubiri milele.

Muda huwa hausongi jinsi tunavyotaka.

Ndiyo sababu lazima usonge kulingana na wakati, Adham.

Sasa hivi, muda hauko upande wetu.

Umeelewa?

Tutapata fursa nyingi za kuvamia.

Itabidi tusubiri wakati mwafaka.

Lililotokea halikuwa sahihi.

Mbona ndovu wa mfalme alipoteza fahamu?

Sielewi chochote.

Lazima mtu alimpa dawa ya kumtia usingizi.

Mbona hili lilitendeka usiku mmoja kabla ya harusi ya Sukanya?

Jodha, lazima umweleze.

Akikasirika, mambo yataharibika.

Mkuu, nimemwandalia Hawai dawa spesheli.

Baada ya kunywa, atapata afueni haraka.

Enda ulete hiyo dawa.

Mimi mwenyewe nitaenda nimpe Hawai dawa.

Leo hii, mnyama mnyonge anahisi maumivu kwa sababu yangu.

Labda nikimguza, nimpapase, maumivu yake yatapungua.

Unaweza kuondoka.

Nakutakia maisha marefu, mfalme!

Nataka kujadili jambo muhimu na wewe.

Mmepewa hurusa ya kuondoka.

Niambie, Adgha.

Nilijaribu kwa uwezo wangu wote. Ni bahati mbaya iliyonikumba.

Sikufanikiwa kupata fununu yoyote kuhusu mshambulizi.

Utapata fununu vipi, Adgha?

Adui anayenilenga sio mmoja tu.

Kuna maelfu ya raia wa ukoo wa Rajput hapa nje.

Kuna askari wangu 5,000 walio miongoni mwao.

Yeyote anaweza kuwa amepanga njama hii dhidi yangu.

Anaweza kuwa adui yeyote wa ukoo wa Rajput au Mughal.

Hata wewe unaweza kuwa adui, Adgha.

Usijali.

Sikushuku, lakini sikuamini wewe pia.

Hata siamini kivuli changu mwenyewe, Adgha.

Malkia Jodha, mbona uko hapa?

Mbona hukuniambia umekuja hapa, malkia Jodha?

Nimekuja kukuomba...

...kuondoka hapa.

Kwa nini?

Licha ya kujua kila kitu mbona unajifanya hujui?

Huoni? Maisha yako yamo hatarini hapa.

Kwanza, ulipokuwa unasafu mashua baharini, kisha hapa kwenye jukwaa.

Umevamiwa kwa kusudi la kukuua.

Toka hapa.

Umeanza kuwa na wasiwasi kunihusu, Malkia Jodha?

Hapana. Nina wasiwasi kuhusu harusi ya Sukanya.

Nina hofu kuhusu Amer.

Chochote kikikufanyikia katika ufalme wa Amer,

...harusi ya Sukanya haitafanyika.

Furaha ya Amer itageuka kuwa huzuni.

Familia yangu itaharibiwa sifa kwa sababu ya hilo janga.

Amer itakumbana na matatizo ya kila aina.

Ndiyo sababu nakusihi. Wewe...

Shukuru Mungu, Malkia Jodha.

Vinginevyo, nilifikiria...

kuwa umeanza kuwa na hofu kunihusu.

Ahsante kwa sababu hukuniruhusu nipoteze imani yangu.

Je, unafahamu?

Maadui zangu hawana kikomo.

Wachache kati yao huja mbele yangu

kuonesha chuki yao na huwa nakubali.

Nina furaha kuwa wewe ni mmoja wa hao maadui ambao huja mbele yangu

na kuonyesha chuki yao.

Vaa vazi hili, Malkia Jodha.

-Nini? -Nimesema ulivae, Malkia Jodha.

Vaa.

Shika sime yangu.

-Unafanya nini? -Shika sime yangu.

Nakufanya wewe kuwa mfalme.

Ili utambue utakavyohisi ukiwa mfalme.

Sasa, wewe ndiye mfalme.

Kiti cha enzi na heshima ya ufalme wa Mughal inategemea wewe.

Mikono yako ndiyo nguvu za sime yako.

Sasa, nitakuomba ujaribu kuelewa mtanziko wangu.

Malkia Jodha, nikitoka Amer, raia

watadhani kuwa niliogopa.

More Swahili subtitles for Jodha Akbar

Komentarze

No comments yet. Be the first to leave one.

Keep it about this subtitle — sync, quality, typos.500 characters left