Jodha Akbar

Jodha Akbar

Pobierz napisy Swahili

Informacje o wydaniu

Jodha Akbar 2013 Episode 025-040 Swahili
Komentarz od kikywebsite

Tagi

other
Opublikowano: 2019-05-18
Pobrania: 22
Dla niesłyszących: No

Podgląd napisów Swahili

Pierwsze 200 wierszy.

Waziri!

Unajua Adham yuko wapi sasa hivi?

Nilimwambia aje hapa. Lazima yuko njiani.

Amelewa.

Anapiga unyende kwa chumba chake.

Anavunja vitu.

Kulikuwa na haja gani ya kukomesha mageuzi huko Mathura?

Adham!

Unafanya nini?

Nilikwambia uje kwa halfa ya Jalal kwa heshima!

-Unakunywa pombe... -Jalal! Jalal! Jalal!

Huwa unataja jina la Jalal kila wakati!

Hafla ya Jalal! Tabia ya Jalal!

Amri ya Jalal! Anachopenda Jalal!

Mimi ni wa maana kwako?

Huwa ninahatarisha maisha yangu na ninapigana vitani kila wakati,

kwa ajili ya Jalal.

Kwa matumaini kuwa siku moja majaaliwa yangu yataanza kufanya kazi.

Lakini malaika wameandika utumwa pekee kwa jaala yangu!

Baada ya kushinda vita, hakuna mtu yeyote alinisifu.

Kwa sababu mamangu mpendwa,

anajali zaidi kuhusu mrithi mtarajiwa wa Jalal.

Lakini hukuwahi kufikiri

kuwa habari hizi zilivunja ndoto zangu.

Nilitamani...

na nikaomba daima, jambo baya limtendekee Jalal,

ili nitawale Agra.

Lakini haki hii ni ya mrithi wake.

Hadi leo, nimetumikia Jalal na mamangu.

Lakini sasa, nitatumikia mrithi wake pia.

Mama, majaaliwa yangu yamebadili nini?

Yamebadili nini?

Je, unajua,

kila nilipoona ukimuunga Jalal mkono,

nilidhani kuwa ulifanya hayo yote, ili uniandalie njia!

Lakini hapana!

Mamangu hanipendi hata kidogo.

Inaonekana kuwa kwa kumchunga Jalal,

umesahau udugu wako wa damu, mama.

Leo katika ufalme wa Mughal, kuna sababu mbili za kusheherekea.

Kwa upande mmoja, Adham Khan alikomesha mageuzi huko Mathura.

Kwa upande mwingine Bi. Ruqaiya

atapatia ufalme wa Mughal mrithi.

Ninawashukuru nyote kwa kuja kwa sherehe hii.

Nitakubali zawadi zenu kwa moyo safi

bila kujali ni kubwa au ndogo kiasi gani.

Kila zawadi ni ya kipekee kwangu.

Anzeni sherehe tafadhali.

Jalal, sasa hivi, hakuna aliye na furaha zaidi yangu katika ufalme huu.

Nilikuagizia Kurani hii takatifu.

Wifi, kwa tambiko hili, vitu hivi vyote vinawekwa

kwa matumaini kuwa kwa namna hii,

utakuwa na mtoto kwa paja lako daima.

Salamu kwa Mfalme na Bi. Ruqaiya.

Tafadhali kubalini zawadi hizi kwa niaba ya Amer.

Bi. Ruqaiya, hii ni zawadi yako

kwa niaba ya baba yetu na Amer.

Kuna zafarani

iliyoagizwa kutoka Kashmir.

Kuichanganya na maziwa na kuinywa

kutafanya mtoto aliye tumboni awe na afya na awe na nguvu.

Ninatumai utakubali zawadi yetu.

Malkia Jodha, wakati kuna nafasi, mbona ushikilie matumaini?

Ningependa wewe mwenyewe uchanganye zafarani kwa maziwa,

na umpatie Malkia Ruqaiya.

Malkia Jodha, ndiyo haya maziwa.

Timiza matakwa ya mfalme.

Subiri Malkia Jodha.

Ninataka kila mtu ajue

kuwa Malkia Jodha amepatiana zawadi hii

kwa ajili ya mrithi wa ufalme wa Mughal.

Hata kama zawadi hii ni ndogo

sababu yake ni muhimu zaidi.

Ninataka Malkia Jodha, achanganye zafarani kwa kutumia kijiko hiki

na amlishe Bi. Ruqaiya, mbele ya kila mtu.

Hakuwezi kuwa na zawadi kubwa, adimu na nzuri zaidi kuliko hii

kwa mrithi wangu ambaye hajazaliwa.

Bado sijakuwa malkia

na Jodha ananitumikia tayari.

Nini kinaweza kunifurahisha zaidi kuliko jambo hili?

Malkia Ruqaiya, kunywa zaidi.

Hii ni nzuri kwa mtoto aliye tumboni.

Anzeni sherehe.

Rahim, nini kimetendeka?

Ninataka kucheza ngoma lakini siwezi.

Mbona mmeacha? Anzeni dansi.

Ninahisi sijatulia.

Nahisi kutapika.

Malkia Ruqaiya, usiwe na wasiwasi.

Unahisi hujatulia kwa sababu ya hali hii.

Utahangaika hivi hadi uzae mtoto.

Usijali.

-Shika. Kula matunda. -Hapana. Sitaki.

Mfalme, hujambo?

-Nina ombi. -Ndiyo?

Umenilea kama mamangu.

Leo nataka usimamie hisani.

Unavyoamuru Mfalme.

Ruqaiya, sherehe imeisha. Ni lazima umechoka.

-Huhisi usingizi? -Hapana Jalal.

Unapopokea baraka kila wakati, huwa huhisi usingizi.

Mungu ametimiza matakwa yako. Utakuwa mama.

Utamwomba nini sasa?

Nizae mvulana.

Sitaki kukupa mtoto tu.

Nataka kukupa mrithi wa ufalme huu.

Nimefurahi sana.

Unajali kuhusu mtoto wangu kuliko unavyonijali.

Nimeanza kumwonea wivu.

Njoo upumzike.

Ninasubiri

wakati ambapo mwanako atacheza

kama vile Rahim amecheza.

Ruqaiya, hebu niambie kitu.

Nini kinakufurahisha zaidi?

Kuwa utakuwa mama au kuwa nitakuwa baba?

Bila shaka, furaha ya kuwa wazazi ni nzuri sana.

Lakini furaha kubwa zaidi ni kuwa ufalme huu utapata mrithi.

Jaala ni kipengele kikubwa sana Ruqaiya.

Nchi huchagua mtawala wake.

Kiti cha ufalme huchagua mfalme wake.

Jalal, acha nchi na kiti cha ufalme vichague

kama mwana wetu atakuwa mfalme au la.

Sasa niambie. Nini kimekufurahisha zaidi?

Bila shaka,

kuwa nitakuwa baba, Ruqaiya.

Ruqaiya, kwa mzazi, mtoto ndiye muhimu zaidi.

Nimeamua kuwa mwaka ujao, sitaenda kwa vita vyovyote.

Nitakaa huku na wewe na mtoto wangu.

Ruqaiya, hii ni neema ya Mungu kwetu.

Ningependa kumshukuru kwa moyo wangu wote kwa ajili ya ukarimu wake.

Jalal, mbona ninahisi kuwa unapatwa na mhemuko.

Ndiyo. Ni kwa sababu jambo hili linahusu mtoto wangu.

Nadhani moyo unapiga kwa kifua changu.

Jalal, umeniita?

Nini kilikuwa cha dharura hadi ukaniita saa hii?

Mama, ninahisia isiyo ya kawaida.

Sijawahi kuhisi hivi. Kutotulia kusiko kwa kawaida.

-Wasiwasi. -Jalal, huhisi vizuri.

Nitatuma daktari wa mfalme aje sasa hivi.

Mama, hakuna haja ya kufanya hivyo.

Jalal, basi niambie unavyohisi.

Hisia ambayo sijawahi hisi.

Ninataka kulala lakini siwezi.

Niko pamoja na kila mtu lakini ninajihisi mpweke.

Nikiwa peke yangu, nahisi kuita kila mtu karibu nami.

Jalal.

Ninajua tatizo lako ni lipi.

Shangazi, niambie mbona ninahisi hivi.

Kwa sababu huwezi kuzuia furaha iliyo ndani yako.

Sijaona Jalal akiwa amefurahi kiasi hiki, kwa muda mrefu.

Hii ni furaha ya kuwasili kwa mrithi wa Ufalme wa Mughal.

Mama huzaa mtoto,

lakini kinababa hupata wasiwasi kuhusu watoto wao.

Ikiwa una wasiwasi kuhusu jambo hili,

basi ni vizuri na hupaswi kuwa na hofuJalal.

Ni neema ya Mungu.

Tuna furaha mno,

baada ya muda mrefu.

Jalal!

Jalal!

Mama, tatizo la Ruqaiya ni lipi?

Jalal, kwa sasa hatuwezi kusema chochote.

Lakini ni hakika kuwa Malkia Ruqaiya anahitaji matibabu sasa hivi.

Lakini kuwepo kwako....

Shangazi, nini kimetendeka?

Jalal...

Malkia Ruqaiya ame...

Shangazi, tafadhali niambie waziwazi, kilichotendeka.

Jalal, mimba ya Malkia Ruqaiya imeharibika.

Nilikuwa nimeishi na ndoto.

Lakini sasa imevunjika.

Mbona Mungu hunitenda hivi?

Mbona huwa ananipa matumaini...

...kisha ananipokonya matumaini hayo?

Ni mwenye huruma sivyo?

Basi mbona hakunihurumia?

Angekuwa mkarimu kwangu na kwa Ruqaiya.

Alikuwa anamwomba kila wakati.

Mbona?

Jalal, ninajua kuwa umeumia sana.

Umevunjika moyo.

Lakini Malkia Ruqaiya amevunjika moyo pia.

Jalal, Mungu ndiye mwenye nguvu zote.

Hakuna mtu yeyote anaweza kujua anachofikiria.

Nikimpata Mungu, nitamuuliza.

Nitamuuliza anachonipangia.

Mama, sijali kama mtu ataninyang'anya taji langu,

kiti changu cha ufalme, ufalme wangu na kila kitu.

Lakini mtu anirudishie mtoto wangu.

Nataka mtu anirudishie mtoto ambaye nimepoteza.

Bi. Ruqaiya, acha nihisi pumzi yako.

Mungu wangu!

Hoshiyar, kaa na malkia.

-Unaweza kusema hivyo kwa uhakika? -Ndiyo Mfalme.

Uharibifu huu wa mimba, haukuwa wa kawaida.

Ni njama ya mtu.

Unajaribu kusema nini?

Maham Anga, malkia alipatiwa kiziduo cha datura .

Mtu yeyote akikunywa hii, atalala.

More Swahili subtitles for Jodha Akbar

Komentarze

No comments yet. Be the first to leave one.

Keep it about this subtitle — sync, quality, typos.500 characters left