لومړۍ 182 کرښې.
Sauti ya mvulana: Kulikuwepo vita zamani sana,
Hata hakuna anayekumbuka.
Giza na woga vilitawala mpaka nyakati za mabaroni,
wanaume na wanawake saba waliounda sheria toka katika machafuko.
Watu waliwakimbilia kwa ajili ya hifadhi.
Na hiyo hifadhi ikawa utumwa.
Walipiga marufuku bunduki na kuyafunza majeshi
ya wapiganaji hatari walioitwa clippers.
Huu ulimwengu umejengwa kwa damu.
Hakuna asiye na hatia hapa.
Karibu badlands. Imetafsiriwa na Nyalusi toka Tanzania.
Mgeni, umepotea?
Mabedui wameushambulia msafara maili mbili hapo nyuma.
Na kuwaua cogs wote isipokuwa mmoja.
Hatujihusishi na kusafirisha binadamu hapa.
Unataka nini?
Msafara huo unamilikiwa na baroni wangu.
Shughulikieni hili suala,vijana.
Tumepata clipper wa ukweli hapa.
Ninyi mbwa huwa hamsafiri katika makundi?
Kwenye sanduku kuna nini?
Hilo halikuhusu kabisa.
Ah!
Mwanaume: Inuka. Inuka.
- Twende zetu! - Muueni!
Ah!
Clipper:Hakuna kwa kwenda mtoto.
Niambie ilikuwaje hadi ukawekwa kwenye sanduku.
tena bila kuuawa kama wengine?
Nina bahati, nadhani.
Kunidanganya ni wazo baya.
Mtu mmoja alisema mjane aliwalipa mabedui ili wanitafute.
Huyo alikuwa wa kwako?
Jina lake anaitwa Sarah.
Hakustahili kufa kwa namna hii.
Kwa hiyo nini kitanitokea?
Nakurudisha kwenye ngome yetu.
Au waweza kuniacha niende.
kwani ungepungukiwa nini?
Utaishi muda mrefu zaidi ukifanya kazi kwenye mashamba ya baroni wangu
kuliko huko nje.
Nitajaribu.
Una jina?
Au unatokea tu, unaua watu na kuondoka?
Kama nikikuambia, utafunga domo lako?
Siwezi kuahidi.
Sunny.
Sunny?
Kwa nini, kwa sababu unaangaza siku ya kila mtu?
Chimba.
Mwanaume: Saba.
Nane.
Tisa.
10.
Moja.
Mbili.
Tatu...
Karibu ngomeni, mtoto.
Mwanaume: Tano.
Moja.
Heshima kwa Rijenti!
Moja!
- Mbili. - Sunny: Njoo.
Tatu.
Nne!
Kuna nini?
Wanaitwa colts. Clippers walio kwenye mafunzo.
Kila mmoja ana fursa kupata vyeo vyetu.
Hapana, asante.
Basi utaishi maisha yako yote ukifanya kazi mashambani.
Haya. Mnakaribia kukutana na baroni.
Anawakaribisha makuruta wapya.
Zamani watu walikichukulia hiki kama kitabu kitakatifu.
Waliamini kina majibu.
toka kwa mungu anayeweza kuwaokoa.
Wavulana, hakuna mungu katika badlands.
Najuaje?
Huyo mungu hawalishi wala kuwavisha
au kuwalinda.
Mimi nafanya hayo yote.
Wengi wenu ni yatima.
Wazazi wenu walifariki baada ya maisha ya utumwa
na kuwaacha ninyi mlipe madeni yao.
Lakini ninawapa njia nyingine.
Wenye nguvu zaidi kati yenu
watapata fursa
kujifunza kuwa clippers.
Baadhi huwaona clippers kama wauaji katili, wasio na mioyo.
Lakini wanaume wanaoijaza ngome hii wako zaidi ya hivyo.
Wao ni familia yangu.
Ukikubalika katika familia yangu,
hakuna familia nyingine.
Wavulana, si lazima muwe watawa wa dini.
Mnaweza kutenda maovu mtakavyo.
Ila utii na bidii ya clipper ni kwa baroni wake.
Hiyo ni sheria yetu ya kwanza.
Malipo yake, mtapata mazuri yote--
chakula, silaha, wanawake.
Njoo hapa, sunny.
Ondoa vesti.
mandhari ilioje, sio?
kila alama inawakilisha uhai,
uhai ambao sunny ameutoa
bila toba, bila majuto.
Kwa kuwa anaua kwa sababu moja,
sababu ipi hiyo, sunny?
Kulinda maslahi yako, baroni.
Hilo lipo sahihi.
Kulinda maslahi yangu, baroni.
nafsi 404, zote zimetolewa kwa ajili yangu.
Hakuna clipper katika badlands
anayeogopwa zaidi, na mtii zaidi.
Huyu mtu anayesimama hapa ni tofauti kabisa
na mtoto mwenye majanga niliyemuona miaka mingi iliyopita.
Sunny aliokotwa akiwa uchi na mwenye kutetemeka.
chini ya mto rabbit,
pasipo wazazi, pasipo historia ya ya nyuma,
bila jina.
Nikagundua kuwa kama Badlands ilikuwa haijamuua,
lazima kuna nguvu ndani yake,
basi nikamchukua,
na kumtengeneza kuwa mtu mnayemuona hapa leo.
Pengine mvulana
atakayefuata nyayo zake
yupo humu ndani.
Je, ni wewe?
Au wewe?
Au wewe?
Sasa nauliza,
mnataka kuwa sehemu ya hii familia?
Wote: Ndiyo, baroni!
Baroni: Mnataka mazuri katika kila kitu?
Wote: Ndiyo, baroni.
Mnataka kuua kwa jina langu?
Wote: Ndiyo, baroni.
Mustakabali wenu umeanza.
Niambie kwa nini mjane anakuhitaji sana.
Sijui, baroni.
Unafahamu kinachowapata watu wanaoficha siri dhidi yangu?
Mpeleke shimoni.
Wacha tuone uwezo wako.
- Mfuatilie huyu mvulana. - Ndiyo, baroni.
Baba, nilikuwa nashughulikia tatizo la mabedui.
Kwa nini ulimtuma sunny bila kuniambia?
Inaonekana mabedui si tatizo halisi.
Mjane alikuwa akiwalipa ili wamfanyie kazi yake chafu.
Baroni mwingine anatupinga.
Kumuua mume wake
hakumfanyi awe Baroni.
Muite vyovyote unavyotaka.
Mazao yetu hayawezi kuchakatwa
bila mafuta yake kwa ajili ya kiwanda.
Unataka kusubiri atuondoe kabisa?
Kama tukimshambulia,tutakuwa tunaanzisha vita.
na mabaroni wengine watano.
Tusipofanya lolote, tutaonekana dhaifu
na watakuja kutuvamia vilevile.
Hatumchukulii hatua yoyote mjane.
Asante, sunny.
Hii nini?
Nirudishie.
Ni yangu sasa.
- We dogo bwege. - Toka.
- Hiyo ni yangu! - Rudi nyuma.
Nipe.
Tokeni hapa.
Kuwa makini.
Watu kama Ajax huanzisha kupigana ili kujionesha kwa maclipper.
Wanataka kuchaguliwa kuwa colts.
Mimi ni bale.
M.K.
Nakulinda, unanilinda.
Jacobee anatuma pole zake.
Ni baron wa tatu kufanya hivyo.
Mimi na wewe tulipooana,
hakuna ambaye angekataa mwaliko
Lydia, ulisema utajitolea kushughulikia mipango ya harusi.
lakini kama ni mzigo mzito sana...
Ah,tafadhali, mpaka hatua hii, wivu umeniisha.
Marry Jade, bibi harusi wako ambaye ni mtumishi wako.
Oa wanawake wengi kadiri utakavyo.
Lydia: Kichwa kinauma tena?
No comments yet. Be the first to leave one.