Первые 120 строк.
Binti Mfalme. Mamake Sultan amepata fahamu.
Razia, ulikuwa wapi?
Ulikuwa wapi, Razia?
Huu ni upuuzi gani? Kwa nini umenileta hapa?
Nahitaji majibu ya maswali yangu.
Fatima.
Binti Mfalme...
Ametuacha sisi sote na kwenda, Binti Mfalme.
Naelewa huzuni ulio nao...
lakini kuwa jasiri.
Itabidi unisaidie.
Lazima tufanye maandalizi ya mazishi.
Wote waliouawa katika tukio hili...
orodha yao lazima itengenezwe.
Kuna damu katika kila pembe ya kasri.
Usemavyo, Binti Mfalme.
Lakini... Binti Mfalme...
Uchungu ulio nao ndani yako, acha utiririke kama machozi, Binti Mfalme.
Angalau omboleza waliofariki.
Machozi yangu yamekauka.
Sina wakati wa kuomboleza.
Chochote nilichosema,
wewe utakitekeleza.
Hukusikia?
Hukusikia nilichosema?
Kisha nilimfanya amwendeshe farasi na farasi akakimbia...
kwa kasi zaidi.
Huna hekima?
Umemfanya mtoto aketi ukingoni mwa ukuta? Angeanguka je?
Nilikuwa makini, bibiye.
Nilikuwa nimemshikilia.
Ni vyema usiseme chochote.
Tayari nina thibitisho la ujuzi wako na hekima.
Tahadhari!
Ulinitenganisha na watu wangu kwa kujihadhari.
Wakati ambao walinihitaji zaidi.
Uliniteka nyara kutoka kwenye kasri,
wakati ambao kila mtu alikuwa anauawa.
-Bibiye wewe ni... -Nashangazwa na ukweli
kwamba licha ya kufanya kosa kubwa hivyo,
badala ya kuondoka kwenye kasri kimya kimya,
kama mtu asiye na adabu, bado uko kwenye kasri.
Twende, Fatima.
Nataka kuwa na muda mfupi na rafiki yangu na mpendwa wangu.
Itakuwa vyema mkiniacha kwa muda mfupi.
Kama unavyoamuru, Sultani.
Samahani, Sultani. Hakim atabaki hapa.
Kwa kuwa kumtunza Sultan Iltumish ni lazima.
Sina pingamizi.
Nasikitika kukuona katika hali hii, Sultan.
Ah Allah!
Kwa nini sikufa kabla ya kuona jambo hili?
Kwa nini Mungu hakuniita?
Hakim Sahib.
Unahisi vipi? Sultani atapona lini?
Ingawa hanjari ni ndogo,
lakini hata jeraha dogo kutokana na hanjari hii iliyo na sumu,
linatosha kumuua Iltumish.
Kusema kweli, sijui ikiwa Sultan Iltumish ataishi.
Majeraha ni makubwa. Itachukua muda kupona.
Asante.
Kwa staha na heshima, kuwa makini!
Mama Malkia, Shamshad Begum anawasili!
Nashukuru mungu,
kwamba mfalme wa Bara Hindi
na rafiki yako yuko hai, Sultani.
Nakuomba kwa unyenyekevu, Sultan,
uongoze msafara wa majeneza.
Tafadhali usiniombe.
Niamrishe.
Si wewe uliye na huzuni tu. Tuna huzuni pia.
Unaondoka?
Lazima niondokoe, Fatima.
Bibiye amesema kweli.
Nilifanya kosa kubwa.
Singemwondoa mahali hapa hivi.
Labda...
Labda yuko hai leo kwa sababu ulimteka nyara.
-Unamaanisha nini? -Mirza...
chochote kinachotendeka, hutendeka kuleta manufaa.
Kusema kweli, ukilifikiria,
kwa kumwondoa mahali hapa, uliyaokoa maisha yake.
Wauaji wangemwona,
hakuna ajuaye kile ambacho kingetendeka!
Hata hivyo nahitaji kuondoka, Fatima.
Mirza amemuumiza Bibiye.
Sasa kazi yangu ni gani hapa?
Hapana, Mirza.
Unawezaje kuondoka hapa katika hali hii?
Licha ya kuona maiti hizi zote,
hajatokwa na machozi.
Usitarajie aomboleze.
Yeye ni mgumu kama jiwe.
Lazima tulivunje jiwe hili, Mirza.
La sivyo, atakufa moyo.
Lazima ayeyuke kwa huzuni kutoka moyoni.
Kisha hisia zitakwisha.
Mirza,
lazima alizwe.
Lazima alizwe, Mirza.
Na kazi hii,
hakuna mwingine ila wewe unayeweza kuifanya.
Mama,
nina wasiwasi kuhusu Razia.
Amekuwa kama sanamu.
Hakuna hata chozi moja linalotiririka kutoka machoni mwake.
Hasemi chochote wala kusikia chochote.
Nina wasiwasi sana juu yake.
Ulipokuwa na nafasi,
kwa nini hukumdunga Sultani Iltumish moyoni kwa hanjari, Shah Turkan?
Kwa sababu penzi lako la kitambo lilirejea?
Kwa nini nimuue aliyekufa tayari, Sultani?
Sultani Iltumish ni mgeni wa siku chache.
Akiuawa leo, maombolezo yataendelea kwa mwezi.
Kisha utahitajika kukaa mbali na Binti Mfalme Razia.
Fikiria.
Labda umesema kweli.
-Ikiwa... -Niachie kila kitu...
na ujitayarishe kwa harusi.
Wabeba jeneza wanakuja kwenye msafara wa mazishi.
No comments yet. Be the first to leave one.