ആദ്യത്തെ 200 വരികൾ.
Nataka kucheza huu mchezo...
...na malkia Jodha.
Nitafurahi kuwa wake wangu wote...
...watacheza huu mchezo.
Ruqaiya akishinda huu mchezo,
sijui atakachomuomba mfalme.
Niambie, malkia Jodha.
Unataka kucheza huu mchezo?
Au unataka kukubali kushindwa bila kucheza?
Hapa nje, huwa hatukubali kifo bila kupigana.
Mwito ukiwa wa vita au mchezo wa sataranji,
sisi Warajput huwa hatujiondoi.
Niko tayari kucheza huu mchezo.
Mchezo wa sataranji unaanza kati ya
malkia mkuu Ruqaiya na malkia Jodha.
Wewe ni mdogo wangu.
Basi utakuwa wa kwanza kucheza.
Kwenye mchezo, sio umri wala hadhi,
lakini ni kucheza huzingatiwa kuwa na maana malkia Ruqaiya.
Iwapo bado unataka niwe wa kwanza kucheza, basi itendeke hivyo.
Na sasa, ngome yako imeondoka.
Na sasa, askofu wako ameshindwa.
Umefanya kosa kubwa sana malkia Jodha.
Nimemzingira mfalme wako kutoka pande zote nne.
Mfalme wako yumo hatarini.
Subiri.
Bado mchezo haujaisha.
Kwa hamu kuu ya kunishinda, wewe mwenyewe umepoteza.
Macho yako yalikuwa kwa mfalme wangu,
na ili kumzingira,
ulimtia mfalme wako hatarini.
Sasa, zamu ni yangu ya kucheza.
Huu ni ushindi.
Hongera. Hongera.
Hongera. Hongera.
Malkia Jodha.
Malkia, kubali hii amri.
Nina furaha sana kuwa kwa baraka za
babangu, mamangu na nyanya, nilishinda huu mchezo.
Lakini sitaki chochote kama malipo.
Nilicheza huu mchezo kama mchezo,
ili kudumisha heshima ya mfalme.
Sitaki ahadi wala zawadi yoyote.
Ukivuta kiko hivi, kitakuwa
na athari mbaya sana kwa koo lako.
Nilishindwa kwenye mchezo wa sataranji.
Sasa wewe utanifunza jinsi ya kufuta kiko changu?
Sikukusudia kusema hivyo, malkia.
Basi ni nini kilitendeka kama alikushinda mara moja tu?
Mungu wangu!
Nirejeshee hiyo.
Hiki kidonda kitakuwa funzo kwako,
ili usiongeze uchungu kwenye jeraha la malkia.
Nenda.
Hasira nyingi sana.
Amenishinda mbele ya kila mtu.
Na katika mchezo wa sataranji.
Ningefikiria kama wewe, basi sijui
ni maisha ya watu wangapi ningekuwa nimeangamiza kufikia sasa.
Najuta kuwa sikuweza kutimiza azimio lako.
Ulitaka kuona nikimfedhehesha mbele ya kila mtu.
Na mimi mwenyewe nilifedheheka.
Nilidhani ingekuwa furaha
nikimshinda huyo malkia wa kihindi kwa rahisi.
Kosa la kwanza ni kumchukulia adui kuwa mdhaifu.
Na mara nyingi hilo huthibitishwa kuwa kosa la mwisho.
Huna majuto yoyote kwa huku kushindwa?
Najuta. Najuta sana.
Lakini sitaonyesha.
Ami Khan alikuwa amenifunza kuwa
kamwe hufai kuacha majuto yako kukuhangaisha.
Usiruhusu watu kujua kuwa ulishindwa na adui wako.
Sherehekea ushindi wako kwa majivuno.
Hii inaitwa siasa.
Ukitilia kushindwa kwako maanani,
basi watu nao watatilia maanani.
Ruqaiya, huwa inapendeza sana kuendesha farasi aliyekuangusha hapo awali.
Sasa, sahau hasira yako, acha mimi nifurahie kiko.
Lakini cha kushangaza ni kwamba alikataa
amri yako kuu iliyokuwa na mhuri wa kifalme.
Huna majuto kwa hilo?
Nitamlazimu kukubali hiyo amri kuu.
Ninataka tu kuona
jinsi ambavyo atatumia hiyo amri kuu.
Kila mtu atege sikio.
Mfalme wa ufalme wa Mughal, mfalme wa India,
mfalme Jalaluddin Mohammad anaingia kwenye kasri!
Mfalme Jalaluddin Mohammad!
Utukufu kwake!
Mfalme Jalaluddin Mohammad!
Utukufu kwake!
Mfalme Jalaluddin Mohammad!
Utukufu kwake!
Mfalme Jalaluddin Mohammad!
Utukufu kwake!
Mwite mkata rufaa.
Niambie.
Unataka nini?
Nataka haki.
Kwenye huu ufalme, kuna mfalme mmoja, bendera moja,
basi mbona kuna sheria tofauti?
Mbona tunalazimishwa kubadili dini yetu?
Naishi kwenye huu ufalme. Nalipa kodi. Sifanyi kosa lolote.
Ukosefu wa heshima.
Huna tabia nzuri kuweza kuongea mbele ya mfalme.
Askari.
Mtoeni hapa mumpeleke korokoroni.
Hapana. Huwezi kufanya hilo.
Wewe ni mfalme wa aina gani?
Alisema nini kibaya?
Sheria ni sawa kwa mfalme na raia.
Ulimuoa malkia wa kihindi.
Hukumlazimu kubadilisha dini yake.
Basi mbona unatufanyia hili?
Una ruhusa ya kuwasilisha rufaa yako kortini.
Hilo halimaanishi unafaa kukosa heshima.
Umefanya uhalifu kwa kumkosoa mfalme kuhusu uamuzi wake.
Ni vizuri.
Malkia mpya atajua jinsi Jalal
hukabiliana na wasiokuwa watiifu.
Hujakosa heshima tu, bali pia wewe ni mhalifu
kwa kuuliza maswali kuhusu uamuzi wa mfalme.
Na adhabu yake ni...
...awekwe korokoroni mara moja.
Nataka watu wasikie vilio vyao.
Mfano unapaswa kuwepo kwa kuwaona.
Ili yeyote asithubutu kumkosea mfalme heshima.
Ukosefu mkubwa wa haki unatendeka hapa.
Mtu aliyekuja kutafuta msaada anawekwa korokoroni.
Ilihali sio kosa lao.
Hata mfalme hakumhurumia mtoto.
Malkia Jodha.
Hakuna haja ya kukasirika.
Hawatoki kwa jamii yetu. Ni watu wa nje.
Unapaswa kuwachukulia watu wa nje kama watu wa nje.
Amri gani inatolewa kwangu?
Adhabu ni ya wahalifu.
Unaweza kurudi nyumbani kwenu.
Nyumba ya aina gani, mfalme?
Majeshi yako yalinyakua nyumba yetu.
Kuna ng'ombe niliyekuwa nikinywa maziwa yake.
Huyo naye walimchukua.
Ndiyo sababu tulikuja kwako.
Kwa sababu mfalme ni Mungu duniani, sivyo?
Uliwatia mamangu na babangu korokoroni.
Nitaende wapi sasa? Nitaishi na nani?
Babako Humayun ni kakangu.
Lakini anataka kuniua kwa sababu ya kiti cha enzi.
Kabla amuue Kamran, nitamuua.
Nitamuua Jalal...
Unafanya nini?
Ondoka malkia, hili ni suala la kisiasa.
Siasa haziendeshwi na watoto.
Kwenye vita kati yenu kaka wawili,
kosa la Jalal asiyekuwa na hatia ni lipi?
Kwanza, ulimtoa kwa babake kwa lazima
na sasa, unataka kumuua?
Hapana, sitaruhusu huyu mtoto asiye na hatia kuadhibiwa.
Malkia!
Ni jeraha dogo tu, Jalal.
Ukilia kwa sababu ya jeraha dogo tu,
utakuwa mfalme vipi?
Silii kwa sababu ya maumivu, nampeza baba na mama.
Kutokana na uwoga wa maadui, sijui
mahali ambapo babako mfalme Humayun na
mamako Hamida Banu wanarandaranda bila kujua pa kwenda.
Lakini uko chini ya ulinzi wangu, mwanangu.
Mimi ni kama babako.
Jalal sio jukumu langu tu, bali ni kama mwanangu.
Kuna nini kama babake na mamake hawako pamoja naye?
Nipo. Mimi ndiye mamake.
Waachilie huru wazazi wa huyu mtoto.
Nyumba, mali na na kila kitu chao kirejeshwe.
Unasema nini? Mfalme huwa habadilishi uamuzi wake.
Adham!
Hakuna anayefahamu zaidi yangu wazazi walivyo muhimu katika maisha ya mtoto.
Anaweza kutwaa dunia nzima bila
wazazi wake, lakini bado atakuwa na upweke kwenye nafsi yake.
Na kila mtu hana bahati kama mimi kumpata mjomba Khan na shangazi.
Sitaki mtoto yeyote kuishi
maisha yake bila mama na babake.
Huenda likawa kosa kwa mfalme kubadili uamuzi wake.
Mimi ni mwanaume mstahiki na mcha Mungu,
nitamrejeshea huyu mtoto wazazi wake.
Na sioni ubaya wowote kwa hili.
Rudi nyumbani kwenu mtoto.
Na umwambie mama na babako kuwa mfalme aliwapa adhabu...
...lakini mtu wa Mungu amewasamehe.
Nadhani muda na hali inabadilika, Nazima.
Kwanza, mchezo wa sataranji ulibadilika,
na sasa, ni uamuzi wa mfalme.
Unachotaka kusema ni nini, Ruksar?
Nilikuwa nafikiri, mbona tusicheze mchezo wa sataranji?
Labda mara hii mimi pia nitakushinda.
Usifikirie kufanya jambo usipokuwa na uwezo.
Unakasirika bila sababu.
Nilikuwa naongea tu kuhusu uamuzi wa mfalme.
Leo hii, mfalme hakubadili uamuzi wake,
kwa sababu huyo mtoto alikuwa wa jamii ya kihindi kama malkia Jodha.
Alibadilisha uamuzi wake,
No comments yet. Be the first to leave one.